WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amempongeza  mhitimu wa DIT Shahada ya Umeme  Erasto Chiswanu aliyebuni na kutengeneza kiti cha walemavu ambacho hakihitaji kusukumwa.

Ametoa pongezi hizo leo alipotembelea kwenye maonesho ya kilele ya Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) 2021 yaliyofanyika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Aidha, Waziri Mkuu amempongeza pia mbunifu mwingine Adamu Kinyekile aliyebuni mashine ya kumsaidia mkulima kuvuta maji, kupukuchua nafaka, kukoboa na kusaga ambayo inatembea na  inamfata mkulima popote alipo.

Mashine hiyo Adamu Kinyekile ametengeneza chini ya usimamizi wa DIT akiwa ni mshindi wa MAKISATU 2019.

Akizungumza wakati akifunga maonesho hayo Waziri Mkuu amesema ameona mmoja wa vijana  ametengeneza kiti cha walemavu."Kumbe  tunaweza kutengeneza kiti cha umeme badala ya cha kuchanganya kwa mikono na hii imefanywa na kijana wa DIT."

Moja ya mtambo wa kumsaidia mkulima kuvuna maji, kupukucha nafaka,kukoboa na kusaga ambayo imebuniwa na kutengenezwa na mhitimu wa DIT .Mtambo huo ni miongoni mwa mitambo ambayo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepata nafasi ya kuona alipotembelea maonesho hayo ya MAKISATU
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza jambo baada ya kutembelea na kukagua mitambo mbalimbali iliyobuniwa na kutengenezwa na baadhi ya wahitimu wa DIT
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...