Mkuu
wa Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, Sadifa Juma (Kulia)
akizungumza na wananchi wakati wa makabidhiano ya vyoo vya Shule ya
Awali, Msingi na Sekondari ya Kandwi iliyoko Unguja, Zanzibar
vilivyofanyiwa ukarabati mkubwa na taasisi ya Asma Mwinyi Foundation
(AMF) kwa hisani ya Benki ya Exim. Wanaomsikiliza ni pamoja na
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Asma Mwinyi Foundation (AMF), Asma
Mwinyi (Kulia kwake), Meneja Mwandamizi wa benki ya Exim Zanzibar,
Mwinyimkuu Ngalima (wan ne kushoto) pamoja na maofisa wengine wa benki
hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, Sadifa Juma akikagua moja ya chumba cha vyoo vya Shule ya Awali, Msingi na Sekondari ya Kandwi iliyoko Unguja, Zanzibar baada ya kufanyiwa ukarabati mkubwa na taasisi ya Asma Mwinyi Foundation (AMF) kwa hisani ya Benki ya Exim.Ukarabati huo umegharimu takriban sh. milioni 10. Wanaoshuhudia ni pamoja na Meneja Mwandamizi wa benki ya Exim Zanzibar, Mwinyimkuu Ngalima (Kulia) na Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Asma Mwinyi Foundation (AMF), Asma Mwinyi (Katikati).

Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, Sadifa Juma akizungumza na wananchi wakati wa makabidhiano ya vyoo vya Shule ya Awali, Msingi na Sekondari ya Kandwi iliyoko Unguja, Zanzibar vilivyofanyiwa ukarabati mkubwa na taasisi ya Asma Mwinyi Foundation (AMF) kwa hisani ya Benki ya Exim.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...