Charles James, Michuzi TV

KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, imemteua Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida, Kenani Kihongosi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama hicho UVCCM.

Kihongosi ameteuliwa kushika nafasi hiyo akichukua nafasi ya Raymond Mwangala ambaye ameteuliwa hivi karibuni na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mkoani Arusha.

Akizungumza na Wandishi wa Habari jijini Dodoma, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka amesema maamuzi hayo yamefanyika leo kufuatia kikao cha kawaida cha Kamati Kuu kilichoketi leo chini ya Mwenyekiti wake, Rais Samia Suluhu Hassan.

Shaka amesema katika kikao hicho pia, Kamati Kuu imempitisha Shekha Mpemba Faki kuwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Konde lililopo Kaskazini Pemba Visiwani Zanzibar katika uchaguzi mdogo utakaofanyika baadae mwaka huu.

" Kamati Kuu imemteua Ndugu Kenani Kihongosi kuwa Katibu Mkuu wa UVCCM, hii ni baada ya aliyekua Katibu Mkuu, Raymond Mwangala kuteuliwa kuwa DC wa Ngorongoro," Amesema Shaka Hamdu Shaka.

Pia Chama hicho kimempongeza Rais Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi kwa namna ambavyo wanafanya kazi vizuri huku wakitekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020/25.

Kenani Kihongosi amewahi kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Iringa, Mkimbiza Mwenge na baadae aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha kabla ya Rais Samia Suluhu Hassan kumteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Singida na leo Kamati Kuu kumteua kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo ya Vijana.

Katibu Mkuu mpya wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi UVCCM, Kenani Kihongosi ambaye ameteuliwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kushika nafasi hiyo, Kabla ya uteuzi huo alikua ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Singida.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...