BABA wa Taifa la Zambia Kenneth David Kaunda amefariki dunia kwa maradhi ya Pneumonia akiwa na umri wa miaka 97, vyombo vya habari nchini humo vimeripoti.
Kenneth Kaunda 'KK' mwanasiasa na mpigania uhuru wa Zambia alikuwa Rais wa kwanza wa taifa hilo na kuliongoza kuanzia 1964 hadi 1991.
Kaunda alikuwa mstari wa mbele kupigania uhuru wa taifa hilo kutoka kwa Waingereza.
Siku mbili zilizopita Kaunda alilazwa katika hospitali moja ya jeshi Mjini Lusaka na kuomba maombi kutoka kwa wananchi wa Taifa hilo kupitia taarifa iliyotolewa na wasaidizi wake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...