Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana na Ajira, Patrobas Katambi akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Benki ya CRDB Kanda ya Kati na vijana wa Bodaboda baada ya kuzindua kampeni ya Tupo Mtaani Kwako msimu wa pili ya Benki hiyo.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana na Ajira, Patrobas Katambi akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Benki ya CRDB ya Tupo Mtaani Kwako leo jijini Dodoma.
Watumishi wa Benki ya CRDB na wananchi mbalimbali wa Jiji la Dodoma wakifurahia uzinduzi wa Kampeni ya Tupo Mtaani Kwako iliyozinduliwa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Kazi Vijana na Ajira, Patrobas Katambi.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kati, Chabu Mishwaro akizungumzia kampeni ya Tupo Mtaani Kwako msimu wa pili ambayo wameizindua leo jijini Dodoma.


 Charles James, Michuzi TV

SERIKALI imesema iko tayari kushirikiana na wadau wa maendeleo zikiwemo Taasisi za kifedha ili iweze kutoa maelekezo kwenye Ofisi za Wilaya na Mikoa kwa ajili ya kuwakutanisha na makundi yote ya Vijana, Wanawake, Walemavu waweze kunufaika.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana na Ajira, Patrobas Katambi wakati akizindua msimu wa pili wa kampeni ya Benki ya CRDB inayoitwa 'Tupo Mtaani kwako'.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Naibu Waziri Katambi ametoa wito kwa Benki ya CRDB kushirikisha Serikali na hasa kupitia Wizara yake ili kuweza kuwakutanisha wananchi na Benki ili kunufaisha pande zote mbili.

Katambi amesema Serikali itaendelea kusukuma sera na sheria na wajibu ilionao ni kuhakikisha Mabenki yote nchini yanashusha riba katika mikopo huku akipoongeza CRDB kwa kufanya hivyo.

" Niwapongeze Sana CRDB mmekua mkishusha riba zenu za mikopo na mmefanya hivyo, huko ni kuwasaidia wananchi hawa na hasa wenye vipato vya chini kujitokeza kwa wingi kukopa na kufanya Biashara ambazo zitanyanyua vipato vyao.

Athari ya kutokutunza fedha wakati mwingine tuna kasumba ambazo  tunazikumbatia wenyewe Mwenyenzi Mungu ametupa fursa nyingi na mabenki mengi lakini sisi hatutaki kuzitumia unapata  100,000 leo kwa dharura unataka kuitumia yote tunza kidogo weka basi hata 50,000 halafu nyingine teketeza hatuna utaratibu wa kutunza fedha,hivyo nitoe rai pia tuwe na utaratibu wa kutunza fedha," Amesema Katambi.

Akizungumzia kampeni hiyo, Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kati,Chabu Mishwaro amesema kampeni ya Tupo Mtaani kwako mwaka jana ilikuwa na mafanikio kwani waliweza kutembelea mikoa 20 na kuwafikia watanzania zaidi ya 100,000.

Chabu amesema msimu wa pili wa kampeni ya 'Tupo Mtaani kwako' unalenga kuhamasisha matumizi ya huduma za  benki pamoja na kuwaunganisha watanzania walio wengi kutumia huduma za Benki ili kuchochea kasi ya maendeleo.

"Tumeenda katika Halmashauri tunatoa fedha kule kama umechukua mkopo nenda CDRD watakusaidia pia wanaweza kukopesha kwa kukuongezea ili ufanye biashara kubwa zaidi pia wamekuwa wakikopesha makundi mbalimbali ya wajasiriamali," Amesema Chabu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...