Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amewaomba madiwani na Wenyeviti wa mtaa kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha jamii katika Suala la usafi.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo katika kikao Cha madiwani na watendaji kata manispaa ya Temeke katika ziara yake ya kujitambulisha na kueleza vipaumbele kwa mkoa wa dar es salaam
ambapo amewaeleza madiwani na watendaji nanma ambavyo haridhishwi na Hali ya usafi Dar es salaam na kuwaomba kumuunga mkono kuiliweka jijii Safi.

Aidha RC Makalla ameeleza mpango wake wa kupendezesha mandhari ya mkoa, kuwapanga vizuri wamachinga na  kuondosha magari mabovu yanayoharibu mandhari ya jiji hilo.

Katika kikao hicho RC Makalla pia amewapa vipaombele vya kushughulikia ikiwemo Ulinzi na Usalama, Usimamizi miradi ya maendeleo, ukusanyaji wa Mapato, utatuzi wa kero za Wananchi na kuimarisha umoja na mshikamano.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...