Na.Vero Ignatus,Arusha

 Sera ya  elimu bila malipo inamaana kwamba mwanafunzi atasoma bila mzazi/mlezi kulipa ada wala michango iliyokuwa ikitozwa shuleni kabla ya kutolewa kwa waraka wa elimu no 5 wa mwaka 2015,ambapo serikali itagharamia mwanafunzi wa shule ya sekondari na bweni iliyokuwa ikitolewa na mzazi/mlezi ambapo walikuwa wanalipa ada na michango mbalimbali.

Sera ya elimu bila malipo ilianza rasmi nchini baada ya serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani mwaka 2015 chini ya hayati Rais Dkt.John Pombe Magufuli.

Sera hii inamaanisha kufutwa kwa ada zote katika shule za sekondari kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne na michango ya wazazi katika ngazi ya elimu ya msingi.

Sera hii imeleta ahueni kubwa kwa wazazi/walezi hasa kulingana na hali duni za kiuchumi za watanzania walio wengi,Hatua hii imeleta tija kubwa katika sekta ya elimu nchini kwani inatoa fursa kwa kila mtanzania kupata elimu ya sekondari na msingi

 Pamoja na sera hii kuleta faida kubwa kwa wazazi lakini imepeleka mzigo mkubwa kwa wakuu wa shule,Wazazi wengi wanadhani kwamba kwa sasa jukumu la kupata elimu kwa watoto wao ni la serikali peke yake.

Upande wa serikali unafanya vyema kutimiza wajibu wake toka sera hii ianzishwe rasmi mwaka 2016. Serikali inatumia fedha nyingi katika utekelezaji wa elimu bila malipo.

Katika kubaini namna ambavyo sera ya elimu imekuwa ikifanya kazi kwa baadhi ya shule za msingi na sekondari wilayani Arumeru mkoani Arusha mwandishi wa michuzi blog aliweza kuzungumza na mkuu wa shule ya sekondari likamba Mwl Juma Tenganija Bwakwimba ambapo amesema elimu bure inawasaidia wanafunzi kuhudhuria masomo yao darasani huku akitegemea ufaulu kuwa mkubwa kwa kuwa bado ni shule changa.

Amesema kuwa elimu bure imekuwa chachu ya kuwafanya wanafunzi kuacha utoro mashuleni kwa kuwa wana uhakika wa kusoma bure bila ya wazazi au walezi kudaiwa michango yeyote.

Kwa upande wake mwalimu Richard Mmassy  kutoka shule ya msingi Likamba iliyopo kata ya Musa wilaya ya Arumeru alisema kuwa kutokana na elimu bure wamekuwa wakifanya vizuri kitaaluma na ufaulu ni mzuri kwa wanafunzi kwani wanafanya vizuri darasani  

Aidha mwandishi wa  blog hii aliweza kuzungumza na baadhi ya wazazi wenye watoto katika shule hiyo ambapo amenukuliwa akisema:

‘’Kuwa wamekuwa wakilipia Pesa ya ulinzi na  chakula hii dhana ya Elimu bure sijaelewa kabisa ,kwenye kikao Cha Wazazi tumeitwa chakula tunalioa 6000 hapo hakuna Elimu bure hayo ,kwa vile wameamua kufanya hivyo waache wafanye wapendavyo Mimi ninachotaka mtoto wangu asome tu’’.Ni maneno ya mmoja wawazazi alilalamika 

Hata hivyo kutokana na kauli iliyotolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa ofisi ya Rais Tamisemi Davide Silinde bungeni Jijini Dodoma inasema kuwa serikali inatoa elimu bila ada siyo elimu bure hivyo wazazi washiriki kutoa michango kwaajili ya maendeleo ya shule 

Nae Waziri wa Elimu Prof.Joyce Ndalichako alisema waraka wa serikali na.3 wa mwaka 2016 ulieleza ushirikishaji wa wazazi katika maendeleo ya shule,lakini shule hairuhusiwi kufukuza watoto kwaajili ya michango

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...