Na.Khadija Seif,Michuzi Tv

PROMOTA maarufu nchini DMK ambae amekuwa akiandaa show mbalimbali nchini za wasanii hasa Muziki pamoja na Filamu  amewataka Mashabiki  wake kutazama show ya Msanii Davido kutoka Nigeria kupitia mtandaoni ili pesa zitakazopatikana zisaidie watoto yatima hapa nchini. 

 Aidha Dmk  ameeleza jinsi ya kutazama show hiyo inayokwenda kwa jina la "Global unity concert itakayofanyika nchini Nigeria  Juni 16 mwaka huu na kwa mara ya Kwanza Msanii Davido ataweza kutoa burudani Mubashara na itawapa fursa waliombali kuona show hiyo kwenye Mtandaoni wa shurtv.

"Show hiyo ya global unity concert utaweza kuiona Mubashara Mtandaoni kwahiyo kwa kupitia kiasi kidogo cha pesa utakacholipia kitakuwezesha kuchangia kabisa kwa watoto yatima wanaoishi katika mazingira magumu".

Hata hivyo Dmk amesema kutokana na yeye kuwa mzoefu kwenye tasnia ya burudani hasa kutafuta Masoko nje ya nchi hivyo tutegemee kuona show ya Zuchu,Alikiba pamoja na Mkali Diamond platinum hivi punde.

"Hivyo tupo kwenye Maongezi na Wasanii wa Nyumbani kwa Sasa na tupo bega kwa bega kutoa support Nyumbani kupitia wasanii wa Tanzania ila kwa Sasa tumeanza na mkali Davido na show itafanyika nchini Nigeria ."

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...