Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam 

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS),katika kipindi cha miezi miwili kasoro limefanikiwa kuweka vinasaba katika lita Milioni 464,215,825 za mafuta na shughuli ya kuweka vinasaba gharama yake kwa lita moja ni shilingi 14 hivyo mpaka sasa wameweza kuingiza fedha kiasi cha shilingi Bilioni 6.5 na fedha hiyo inaingia moja kwa moja serikalini.

Ameyasema hayo leo Mkuu wa Shughuli za Uwekaji Vinasaba Mhandisi Florian Batakanwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Shirika la Viwango (TBS) leo Jijini Dar es Salaam.

Amesema shughuli ya kuweka vinasaba katika mafuta inawekwa kwenye maghara yanayopokea mafuta bandarini ambayo kwa Dar es Salaam kuna maghala 19 ambayo wamekabidhiwa na EWURA na mkoani kuna maghala matatu lakini pia kuna maghala mawili yameongezeka hapa jijini na kufanya kufikia 21 kwa Dar es Salaam.

"Zoezi hili mwanzo lilikuwa linafanywa na taasisi isiyo ya kiserikali hivyo mapato yote haya yalikuwa yanaenda kwenye taasisi hiyo na serikali ilikuwa inapata kodi kwenye taasisi hiyo'. Amesema Mhandisi Batakanwa.

Aidha Mhandisi Batakanwa amesema hii zoezi la kuweka vinasaba kwenye mafuta lina uhusiano mkubwa na usalama wa nchi kwani mtu ama kampuni binafsi akiweza kugawa vinasaba kwa watu wasiohusika nchi inakuwa inateteleka kwasababu kiuchumi inakosa mapato yake.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...