Leo Julai 2, 2021 wadau mbalimbali wametembelea Banda la Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) . Kupitia maonesho hayo, GST imeendelea kuwaelimisha na kuwafahamisha juu ya masuala mbalimbali ikiwemo aina za madini na miamba inayopatikana katika maeneo mbalimbali ya nchi; huduma zitolewazo na GST;  na njia za kisayansi zinazotumika katika  utafutaji, uchimbaji na uchenjuaji Madini.

Aidha, katika msimu huu wa Sabasaba GST inatoa huduma za utambuzi wa madini  kwa kutumia vifaa vya kisasa vilivyopo katika Banda lake. Pia, ushauri wa namna bora ya kutafuta na kuchenjua madini unatolewa .   Vilevile,  Banda la GST  linaonesha madini mbalimbali yanayopatikana nchini ikiwa pamoja na Madini pekee  ya Tanzanite.
Kauli Mbiu ya Maonesho ya mwaka wa huu wa 2021 inasema "Uchumi wa Viwanda Kwa Maendeleo ya Ajira na Biashara Endelevu"









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...