
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Patrobas Katambi (wa pili kushoto), akimkabidhi cheti cha shukrani Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Letshego, Simon Jengo (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, Andrew Tarimo (wa pili kulia) kwa udhamini wa Kongamano la Biashara na Uchumi lililofanyika jijini Dodoma, jana. Wengine ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Mayoda Economic Development Group, Sophia Simbu (kushoto) na Mwenyekiti Mtendaji wa Mayoda, Agustino Matefu.

Meneja wa Uendelezaji Biashara Benki ya Letshego, Ruth Mpangalala (kushoto) akifafanua jambo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Patrobas Katambi (kulia) mara baada ya kufungua Kongamano la Biashara na Uchumi lililofanyika jijini Dodoma, jana. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, Andrew Tarimo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...