Na Mwamvua Mwinyi,Mafia
MKUU
wa wilaya ya Mafia ,mhandisi Martin Ntemo ,ameuagiza wakala wa ufundi
na umeme (TEMESA ) pamoja na mamlaka ya Bandari (TPA ) kuhakikisha
wanashughulikia kero zinazolalamikiwa katika kivuko na Bandari ,ikiwa ni
pamoja na kupitia upya nauli zinazotozwa kuwa kubwa kuliko uhalisia.
Aidha ,nauli itakayopangwa ipitishwe na mamlaka zenye dhamana ya kupanga viwango vya nauli katika vyombo vya usafiri.
Akitoa
maelekezo hayo katika mkutano wa wadau uliohudhuriwa na mbunge wa Mafia
Omar Kipanga ambapo wadau waliwasilisha kero zao kwa ujumbe wa TEMESA
ili kufuatilia maelekezo ya Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi
aliyoyatoa Julai 2021,alipotembelea eneo la Nyamisati ambako kivuko
hicho huanzia safari zake kuelekea Mafia.
Mkuu
wa wilaya hiyo Ntemo baada ya kupokea michango mbalimbali ya wadau
,alieleza kero hizo zimekuwa zikilalamikiwa kipindi kirefu hivyo
kusababisha kudidimia kwa uchumi na maendeleo ya wilaya.
Ameiagiza
TEMESA pia wakati ikipeleka timu ya ufuatiliaji maelekezo ya Naibu
Waziri wa Ujenzi wahakikishe kero zilizotolewa na wadau zinafanyiwa kazi
.
Hata hivyo ,aliwataka
kufungua ofisi za kusimamia shughuli za kivuko na kukatia tiketi kwa
upande wa Mafia na Nyamisati na mashine za kukatia tiketi ziongezwe.
Nae Kipanga ameeleza ,tayari amewasilisha barua na kumkabidhi mtendaji mkuu, ikielezea maeneo yenye kero.
Wakati huo huo ,Ntemo
amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Ujenzi wa chuo cha VETA
ambacho ujenzi wake uko katika hatua ya kukamilika.
"Chuo
hiki ni sehemu ya mradi wa serikali wa Ujenzi wa vyuo 25 vya aina hii
vinavyojengwa katika wilaya mbalimbali kwa gharama ya sh .bilioni 1.6
kwa kila chuo"
Ntemo
pia alipitia ofisi za TANESCO kujionea mitambo inayozalisha umeme
ambayo ndio chanzo cha nishati ya umeme wilayani humo ,ambapo Mafia
inapata umeme unaozalishwa kwa mtambo wa dizeli .
Katika
eneo hilo zipo jenereta tano zenye uwezo wa kuzalisha kilowatts 624
kila moja zote pamoja zikiwa na uwezo wa kuzalisha kilowatts 3,120
ikilinganishwa na mahitaji ya wilaya hiyo kilowatts 1,520 .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...