Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imeibuka kidedea kwa kuwa Mshindi wa pili kwenye kundi la Wadhibiti kwenye Maonesho ya Sabasaba mwaka 2021. 

Akizungumza baada ya ushindi huo Mkuu wa kitengo Cha Masoko na Uhusiano kwa Umma, Shamim Mdee amesema PSPTB imekuja kivingine mwaka huu kwa kuja na Ubunifu mpya katika masuala ya Ununuzi na Ugavi ndio maana imeshika nafasi nzuri katika Tuzo hizo za Maonesho ya mwaka huu.

Mdee amesema Ushindi huo umepatika baada ya kukidhi vigezo mbalimbali vya ushindi ikiwemo ubora wa banda (branding), Ubunifu, Huduma bora kwa wateja na utoaji bora wa Elimu.

Katika kundi hilo mshindi wa kwanza amekuwa Benki ya Tanzania (BOT) na mshindi wa tatu Mamlaka ya Udhibiti ya Huduma za Nishati na Maji (EWURA).
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa PSPTB, Paul Bilabaye (wa tatu kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa PSPTB wakiongozwa Mkuu wa kitengo Cha Masoko na Uhusiano kwa Umma, Shamim Mdee(wa pili kulia) kwenye banda la Bodi hiyo kwenye maonesho ya Sabasaba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...