Na Mwamvua Mwinyi,Pwani


Mkuu wa Mkoa wa Pwani ,Abubakar Kunenge, amesema hatosita kumchukulia hatua kali ya kisheria yeyote yule atakaefanya uvamizi wa ardhi wa aina yeyote.

Alieleza hayo wakati wa kuzindua Kampeni ya kushughulikia Migogoro ya  Sekta ya Ardhi Mkoani  Pwani,uzinduzi uliofanyika Mjini Kibaha,uliomshirikisha William Lukuvi, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Kamati ya Usalama ya Mkoa.

Alieleza kuwa watafanya ziara na  Waziri wa Ardhi katika Wilaya za Kibaha, Bagamoyo, Mafia, Mkuranga, Rufiji na Kibiti kuanzia Tarehe 14 Julai,2021  hadi Tarehe 22 Julai 2021 kushughulikia na kutatua Migogoro ya Ardhi.

Kunenge, aliwataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wote Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanatumia nafasi zao katika kutatua migogoro ya Ardhi.

Kunenge pia aliwataka Viongozi hao wa Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanaboresha Daftari la makazi na kuhakiki idadi ya mifungo iliyopo mkoani Pwani ili kuepukana na Migogoro ya Ardhi.

Naye Waziri Wa Ardhi  Lukuvi kwa Upande wake amewataka Wakuu wa Wilaya  kuhakikisha wanatatua migogoro ya Ardhi na wasisubiri mpaka wananchi waje kulalamika kwa Viongozi wakuu,

Aliziagiza Halmashauri zote Tanzania kuhakikisha wanazisimamia kampuni binafsi za upimaji wa ardhi na wasiziache zikafanya kazi zenyewe.

“Kampuni Binafsi lazima zisimamiwe na zisiachwe zifanye kazi zenyewe kwani msimamizi wa Ardhi katika Halmashauri ni Halmashauri” alisema Lukuvi.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...