Tasisi ya kifedha  ya kukopa na kuwakwamua  wajasiliamali na wafanyabiashara nchini ,MMJ Microfinance imezinduliwa leo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa sherehe ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo na Uzinduzi rasmi,Mkurugenzi wa tasisi Bi. Esther Ogutu alisema ni furaha ilioje kufanikisha ndoto zake za kumiliki na kuongoza taasisi hiyo kwani ni changamoto nyingi wanapitia wanawake katika kusimamia taasisi za kifedha nchini.

Akifafanua zaidi alisema moja ya changamoto hizi ni pale wakopaji wanapokuwa hawana elimu ya kutosha katika masuala ya kifeza na kujikuta wanatumia pesa za mikoapo kwa kufanya shughuili nyingine za kifamilia badala ya mkopo kwa ajili ya biashara ili kujikwamua.

Pia aliwataka wajasilia mali kujenga tabia ya kuwa na nidhamu ya fedha za biashara ili kujikwamua na kuweza kutimiza  malengo.

Kwa upande wa wadhamini wakuu na wadau wa taasisi hiyo Benki ya CRDB, Meneja biashara wa Benki hiyo tawi la PTA Anande Mwasha aliwataka wafanyabiashara nchini kujenga tabia ya kukopa katika taasisi za kifedha .

kwani kufanya hivyo kunaongeza mtaji na kufanikisha malengo kwa wakati ,pia aliwaambia kuwa wafanyabiashara wakubwa duniani mikopo ya taasisi za fedha ndio imefanikisha malengo yao hivyo kutoogopa kukopa.

Mkurugenzi wa Tasisi ya kifedha ya MMJ Microfinance, Esther Ogutu (wa pili kushoto) na Meneja biashara wa CRDB tawi la TPA,Anande Mwasha (katikati) wakikata  utepe wakati wa uzinduzi wa  taasisi hiyo  ya mikopo uliofanyika jijini Dar es Salam.

Meneja Mwendeshaji wa tasisi hiyo Miltone Obonge akizungumza wakati wa uzinduzi huo
Baadhi ya Wajasiliamali wakiwa katika hafla hiyo
Wajasiliamali wakifatilia
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...