Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amesema atafanyia kazi vilio vya wachimbaji wadogo katika mgodi wa Imalamate, ambao wameomba uongozi wa Wilaya ya Busega kupeleka huduma ya nishati ya umeme na kujenga barabara itakayowezesha kuboresha mazingira ya mgodi huo, hivyo kuongeza uzalishaji. Mhe. Gabriel Zakaria ameyasema hayo tarehe 26 Julai 2021 alipotembelea mgodi huo kusikiliza kero za wachimbaji wadogo.

Katika kikao hicho, Mhe. Gabriel Zakaria ameweza kusikiliza kero zilizopo katika mgodi huo, huku akisisitiza kwamba kero zilizobainishwa zitatatuliwa kwani anapenda kuona kila mchimbaji katika mgodi huo anapata haki yake. “Mimi ni mhubiri wa amani na haki, hivyo sitopenda kuona mnakosa haki yenu kwani wote mnatafuta” aliongeza Mhe. Gabriel Zakaria.

Mhe. Gabriel Zakaria amesema amesikia vilio na kero za wachimbaji wadogo, hasa kero ya kutokuepo kwa umeme wa uhakika na miundombinu mibovu ya barabara, hivyo amesema atahakikisha huduma ya nishati ya umeme inafika katika mgodi huo. “NItaongea na na TANESCO ili kufanikisha huduma ya nishati katika mgodi huo” alisema Mhe. Gabriel Zakaria. Aidha, Mhe. Gabriel Zakaria amewatoa hofu wachimbaji wadogo, na kusema kwamba anaelewa changamoto zinazowakabili wachimbaji hao ikiwemo ya kukosa huduma ya nishati ya umeme ambayo inasababisha kuwepo kwa uzalishaji mdogo na wizi hasa nyakati za usiku.

Kero nyingine zilizobainishwa na wachimbaji hao ni pamoja na tozo na kodi kubwa, kutofanyika kwa mnada kwa wakati, na matukio ya uhalifu nyakati za usiku. Akijibu Sehemu ya kero hizo Afisa Madini Mkoa wa Simiyu Mhandisi Amini Msuya amesema kuwa mchimbaji yeyote atakayepata kero au changamoto awasilishe malalamiko katika vyombo vinavyohuskia ikiwemo Ofisi ya Madini Mkoa, na malalamiko yatafanyiwa kazi kwa wakati.

Kwa Upande miwngine Mhandisi Msuya ameweza kutoa ufafanuzi wa mgawanyo wa mifuko ya mchimbaji, akisema kwamba asilimia 70 ya mifuko ni mali ya mchimbaji, wakati asilimia 20 ni ya kampuni yenye leseni na asilimia 10 ni mali ya mwenye shamba, huku akiwataka wamiliki wa leseni kutozidisha asilimia za mgawanyo wa mifuko kwani kufanya hivyo ni kukiuka utaratibu na miongozo.

Mhe. Gabriel Zakaria kwa mara ya kwanza ametembelea mgodi wa Imalamate huku akiweka dhamira ya kutatua kero za wachimbaji wadogo, ambapo mgodi huo una zaidi ya wachimbaji wadogo 5,000. Mhe. Gabriel Zakaria amesema iili kutengeneza mazingira bora ya kufanyia kazi, ni lazima malalamiko ya wachimbaji wadogo yafanyiwe kazi, lakini pia kuboresha miundombinu katika mgodi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...