Waziri wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo (kulia), akisaini kitabu cha wageni alipofika katika banda UTT AMIS lililopo ndani ya Banda la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF). Katikati ni Afisa Mkuu wa Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya UTT AMIS, Martha Mashiku.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo (kulia), akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mkuu wa Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya UTT AMIS, Martha Mashiku, juu ya fursa za uwekezaji zinazopatikana katika kampuni hiyo.

Afisa Mkuu wa Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Martha Mashiku, akitoa maelezo kuhusu fursa zilizopo katika mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja kwa mwananchi aliyefika katika banda la kampuni hiyo kwenye Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Waziri Ramadhani, akitoa vipeperushi vya taarifa za fursa zilizopo katika mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Temboni waliotembelea banda la kampuni hiyo kwenye Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...