Katibu Tawala Msaidizi, Uchumi na Uzalishaji  wa Mbeya, Said Maditto ( kushoto), akizungumza na wauza pembejeo za kilimo wa Mkoa wa Mbeya na Songwe na wadau wengine wa mbolea ya Yara wakati wa uzinduzi wa programu ya yaraConnect mjini Mbeya leo. Alimwakilisha mkuu wa mkoa huo katika uzinduzi huo. Kushoto kwake ni Bwanashamba Mwandamizi wa Yara, Maulidi Mkima, Meneja Biashara Kanda ya Kusini, Andrew Ndundulu na Meneja Masuluhisho ya Kidigitali wa Yara, Deodath Mtei.

Katibu Tawala Msaidizi, Uchumi na Uzalishaji  wa Mbeya, Said Maditto (katikati) waliokaa, Bwanashamba Mwandamizi wa kampuni ya mbolea ya Yara Tanzania, Maulidi Mkima (kushoto),  na  Meneja Biashara wa Yara Kanda ya Kusini , Andrew Ndundulu, wakipiga picha ya pamoja wauza pembejeo za kilimo wa Mkoa wa Mbeya na Songwe na wadau wengine wa mbolea ya Yara baada ya uzinduzi wa programu ya yaraConnect mjini Mbeya.

Meneja Huduma kwa Wateja Kidigitali wa Kampuni ya Mbolea ya Yara, Eva Sauwa (kulia), akitoa maelekezo kwa  mmoja wa wauza  pembejea za kampuni hiyo katika hafla ya uzinduzi wa programu ya yaraConect kwa Mkoa wa Njombe ambapo pamoja na mambo mengine wauzaji hao wa pembejeo za yara walipewa mafunzo mbalimbali ya matumizi ya programu hiyo na masuala mengine ya kitaalamu kuhusu kilimo na jinsi watakavyoweza kuwasaidia wakulima ambao ndio wateja wao kitaalamu. Hafla hiyo ilifanyika mjini Njombe jana.

Meneja Masuluhisho ya Kidigitali wa Kampuni ya Mbolea ya Yara, Deodath Mtei (wa pili kushoto), akitoa maelekezo kwa  mmoja wa wauza  pembejea za kamupuni hiyo katika hafla ya uzinduzi wa programu ya yaraConect kwa Mkoa wa Njombe ambapo pamoja na mambo mengine wauzaji hao wa pembejeo za yara walipewa mafunzo mbalimbali ya matumizi ya programu hiyo na masuala mengine ya kitaalamu kuhusu kilimo na jinsi watakavyoweza kuwasaidia wakulima ambao ndio wateja wao kitaalamu. Hafla hiyo ilifanyika mjini Njombe jana.

Katibu Tawala Msaidizi, Uchumi na Uzalishaji  wa Mbeya, Said Maditto, akizungumza na wauza pembejeo za kilimo wa Mkoa wa Mbeya na Songwe na wadau wengine wa mbolea ya Yara wakati wa uzinduzi wa programu ya yaraConnect mjini Mbeya leo

Meneja Masuluhisho ya Kidigitali wa Kampuni ya Mbolea ya Yara, Deodath Mtei akizungumza na wauza pembejeo za kilimo wa Mkoa wa Mbeya na Songwe na wadau wengine wa mbolea ya Yara wakati wa uzinduzi wa programu ya yaraConnect mjini Mbeya leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...