Katika kumkomboa mtoto wa kike ili aweze kufikia malengo yake Shirika linapojishughulisha na masuala mbalimbali ikiwemo kutoa mikopo kwa wanawake, kutoa elimu ya miradi  BRAC Maendeleo Tanzania limetoa vyeti kwa wanafunzi   86 ambao wamehitimu  Mafunzo ya kozi fupi  mbalimbali za ufundi stadi.

Mafunzo  hayo yanayotolewa bure walengwa zaidi ni  watoto wa kike ambao wamepata fursa kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo Mapishi, urembo, Upambaji na  ushonaji.

Akizungumza katika mahafali ya kuwatunukia vyeti wanafunzi hao, Mkurungezi wa BRAC International Afrika, Lucy Okowa amewataka wahitimu hao kutumia vyema Mafunzo waliyoyapata ili waweze kutimiza ndoto zao.

Okowa amesema wanafunzi hao wamenuafaika  na Mafunzo hayo chini ya mradi  wa Ela ambao umelenga kumyanyua mtoto wa kike na kumuwezesha kumudu maisha yake kiuchumi na kijamii  na kufanikiwa kumaliza mafunzo na kupata msaada wa vifaa mbalimbali

Amesema wanawake duniani kote wamekuwa wakisifika kwa kuwa watu wenye ustahimilivu na kujitolea kwa nguvu zao zote katika kuhakikisha familia zao zinasonga mbele.

"BRAC ina amini kuwa ili kuleta mabadiliko chanya katika jamii na kuinua familia kwa ujumla ni muhimu kumwezesha mwanamke kwa sababu daima mwanamke hashindwi na jambo"amesema

Aliwasihi wahitimu hao wanapoanza safari ya ujasiriamali wawe makini ikiwa ni pamoja na kuzingatia Mafunzo mbalimbali waliyoyapata katika kipindi chote cha mafunzo.

"Ujasiriamali sio lelemama nawaomba muwe wavumilivu chagamoto nyingi mtapitia lakini msikate tamaa  kila unapofeli nyanyuka, jifunze kutokana na makosa na uendelee kukaza mwendo kwa sababu wanawake sio jadi yetu Kushindwa"alisisitiza Okowa

Elina Patrick ni mmoja wa wanafunzi walionufaika na Mafunzo hayo katika eneo la Upambaji amesema Mafunzo aliyoyapata yatamsaidia kujikwamua na kujiajiri mwenyewe na kumuwezesha kupata kipato cha kumudu maisha yake.

"Matarajio yangu ni kufungua salooni yangu mwenyewe ambayo itanisaidia kutegeneza kipato changu mwenyewe "amesema

Naye Habiba Sangasi alilishukuru Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania kwa kumuwezesha kupata ujuzi uliokuwa ni ndoto yake katika maisha yake.

Mkurugenzi wa upande wa Africa kutoka BRAC International Bi. Ruth Okowa akisikiliza jambo kutoka kwa mmoja wa mabinti wanaonufaika na mradi wa ELA unaotekelezwa na BRAC Maendeleo Tanzania. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa BRAC Maendeleo Tanzania, Bi Susan Bipa
Mkurugenzi wa upande wa Africa wa BRAC International Bi. Ruth Okowa akikabidhi vifaa vya ujasiriamali kwa mmoja wa wasichana 86 ambao walipewa vifaa hivyo katika hafla iliyofanyika katika Chuo cha Ufundi Temeke.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...