Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

TIMU ya Kampala International imeingia hatua ya 16 bora baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya timu ya Zofa FC  kwenye mashindano ya Ndondo CUP  katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Bandari Temeke Jijini Dar es Salaam na sasa wanaendelea kujipanga katika hatua hiyo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Kocha wa timu hiyo John Marwa amesema wamejipanga kufanya vizuri baada ya kufikia mafanikio hayo na wameingia hatua hiyo kwa idadi ya mabao waliyoyapata kuanzia michezo ya awali  na hivyo kuingia 16 bora.

"Unajua timu yangu tangu tumeanza hatua ya michezo hii ya Ndondo CUP tulikuwa tumepanga kuingia katika hatua hii  ya timu 16 hivyo malengo yametimia sasa tuna angalia michezo iliyopo mbele yetu," amesema Marwa.

Amesema ilikuwa si kazi rahisi kuifunga timu ngumu ya Zofa FC ila waliweza kuwafunga licha ya wapinza kuwa na baadhi ya wachezaji wanaocheza Ligi Kuu Tanzania Bara.

Aidha amesema kuwa  wao Kampala Inter  ushindi wao huo   umechochea mafanikio mapya katika ushiriki wao kwani timu yao ndio kwanza imeshiriki mashindano hayo kwa mwaka huu.Kocha huyo amesema kuwa kwa kuwa katika mchezo huo uliopita walijikuta wanawatuliza vizuri wachezaji wa timu hiyo pinzani kwa kuongeza bidii na nidhamu uwanjani.

Kampala Inter ambao ni wanafunzi wa chuo cha elimu ya juu nchini tayari imeonesha kuwa hawajaingia kwenye mashindano hayo kutaka kujaribu tu baahati yao bali tayari wametoa taarifa kuwa timu imeishaanza kujifua katika uwanja wao wa Chuo chao kilichopo maeneo ya Gongolamboto Dar es Salaam ili kujiwinda na michezo ijayo.

Wanafunzi hao wanaobukua kitabu  Chuo cha Kampala  kabla ya kuiondoa Zofa rekodi zao ni muruwa  kwani awali walishatoka sare pia na timu ngumu ya Kinondoni UTD katika mchezo wa Ndondo Cup uliochezwa Julai 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa Kinesi Dar es Salaam..

Kampala ilianza kwa kishindo kwa kuibuka na ushindi wa mabao kuibuka na ushindi wa mabao 3_1 dhidi ya majohe UTD katika mchezo wa hatua ya 32 bora uliochezwa kwenye Dimba la Bandari Temeke, Dar Es Salaam.

Mweenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Ndondo CUP 2021 Shaffih Dauda awali kuelekea kuanza rasmi kwa mashindano hayo alitangaza habari  za msimu huu ambapo kwenye upande wa zawadi mshindi wa kwanza ataondoka na kitita cha pesa taslmu Sh.Milioni 20 .

Zawadi kwa mshindi wa pili wa mashindano   zimetajwa kuwa ni Sh.Milioni 10 ambapo timu zilizoshiriki nusu fainali kila timu itapata Sh.Milioni 2.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...