NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA
MKUU
wa wilaya ya Kibaha ,mkoani Pwani ,Sara Msafiri ametoa siku tano kwa
wafanyabiashara ndogondogo wa Soko la Picha ya Ndege ,waliogoma kuondoka
katika eneo la hifadhi ya barabara ili kumpisha mkandarasi aendelee na
ujenzi wa barabara kuu .
Akizungumza
na wafanyabiashara hao,wakati wa ziara ya kamati ya siasa ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM ), Kibaha Mjini ,Msafiri alieleza amesikia wapo vinara na
baadhi ya wafanyabishara wanadaiwa kuchochea kushinikiza
wafanyabiashara wengine wasihame katika eneo lililotengwa.
Msafiri
alisema wafanyabiashara walitakiwa kuhamia , eneo la shirika la elimu
ambalo lipo river road Msufini lakini wamekaidi na kudai kuwa hakuna
wateja na wengine wamekosa vizimba.
"Hili
eneo ni hatarishi na Tanroad walishawaelekeza mhame ili mkandarasi
aendelee na ujenzi ,mnatakiwa mhame pia kwa usalama wa maisha yenu
kujilinda na ajali "
Msafiri ameeleza ifikie hatua jamii ikaacha kuingiza masuala ya siasa katika maendeleo .
Nae mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini ,Maulid Bundala alisisitiza wafanyabiashara waliogoma kuondoka.
Bundala
alisema ,katika masuala ya kijamii na maendeleo watu waache kuingiza
siasa na uchama hali inayokwamisha juhudi za serikali .
Awali
mmoja wa wafanyabishara hao ,Anelista Mbaga alibainisha mgogoro huo ni
wa muda mrefu,mwanzo walitakiwa kuhamia eneo la Lulanzi ambako waliona
ni mbali , baadae wakatakiwa kuhamia eneo la River road ambako wachache
wamegomea .
Mbaga alieleza ,yeye na baadhi wametii kuhama lakini hawapati wateja kwani wote wanaishia kwa wafanyabiashara wa barabarani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...