Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja (kushoto) wakitazama magogo katika kijiji cha Wachawaseme ambayo yamevunwa kinyume cha utaratibuna watu wasiojuliakana kutoka katika Pori la Akiba la Igombe wilayani Kaliua mkoa wa Tabora, Agosti 28, 2021. Waziri Mkuu aliiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kuyapiga mnada magogo hayo kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na serikali. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mipaka ya Hifadhi ya Iswima katika Pori la Akiba la Igombe wilayani Kaliua ambako aliagiza pori hilo lilindwe baadwe baada ya kushuhudia uharibifu unaofanywa na watu wanokata miti, kuendesha shughuli za kilimo, uvuvi na makazi kinyume cha sheria, Agosti 28, 2021.. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mipaka ya Pori la Akiba la Igombe wilayani Kaliua ambako aliagiza pori hilo lilindwe baada ya kujionea uharibifu unaofanywa na watu wanokata miti, kuendesha shughuli za kilimo, uvuvi na makazi kinyume cha sheria, Agosti 28, 2021. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Balozi. Dkt. Batilda Burian. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mipaka ya Pori la Akiba la Igombe wilayani Kaliua ambako aliagiza pori hilo lilindwe baada ya kushuhudia uharibifu unaofanywa na watu wanokata miti, kuendesha shughuli za kilimo, uvuvi na makazi kinyume cha sheria, Agosti 28, 202. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Dkt. Batilda Burian. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...