Na Amiri Kilagalila,Njombe

Ili kuendelea kukabiliana na changamoto ya ugonjwa wa Corona,mkoa wa Njombe umepokea dozi 30,000 ya chanjo ya corona itakayoweza kugawanywa katika halmashauri zote za mkoa wa Njombe kwa awamu ya kwanza huku makundi kadhaa yakianza kwa kupewa kipaumbele.

Akizungumza na vyombo vya habari mkoani hapo,mkuu wa mkoa wa Njombe mhandisi Marwa Rubirya amesema mkoa huo utaanza zoezi la kutoa chanjo hapo kesho mara baada ya uzinduzi utakaofanyika katika hospitali ya rufaa iliyopo wikichi mjini Njombe.

“Tumepata dozi elfu 30,000 na ni chanjo aina ya Johnson & Johnson na kama taifa zipo chanjo kama aina tano ambazo zimeainishwa kutumika hapa nchini.Kwa hiyo mapema leo asubuhi tumepokea dozi elfu 30,000 ambayo leo tunasambaza maeneo mbali mbali katika mkoa wetu na kesho asubuhi tunakwenda kuzindu zoezi hili la kutoa chanjo na mimi mwenyewe nimeridhia na nitakuwa wa kwanza”alisema Marwa Rubirya

Katika hatua nyingine Rubirya ametoa wito kwa wananchi walio tayari kuweza kujitokeza kwa ajili ya chanjo hiyo kwa kuwa ni salama.

“Nihamasishe wananchi wote ambao watakuwa wamepata nafasi katika hii awamu ya kwaza kufika na kupata chanja kama ambavyo wataalamu wetu wa afya wameshadhibitisha”alisema Rubirya

Dkt,Zabron Masatu ni mganga mkuu wa mkoa wa Njombe ametaja vipaumbele vya makundi yanayotakiwa kuanza kupata chanjo huku akitaja mahitaji ili kupata chanjo hiyo ikiwemo kujisajili kwenye mtandao wa wizara ya afya au kufika kwenye kituo kwa kuwa na kitambulisho cha nida au cha kupigia au leseni ya udereva kwa ajili ya utambulisho.

“Kipaumbele cha kwanza ni kwa watoa huduma kwenye sekta ya afya wale wote walioajiriwa na serikali na wanaofanya kwenye sekta binafsi,kipaumbele cha pili ni watu wazima kuanzia umri wa miaka 50 na kuendelea na kipaumbele cha tatu ni kwa watu wenye magonjwa sugu”alisema Dkt,Zabron Masatu

Miongoni mwa vituo vya afya vitakavyotoa chanjo kwa mkoa wa Njombe ni Kituo cha hospitali ya mkoa wikichi,hospitali ya kibena pamoja na kituo cha afya cha Uwemba kwa halmashauri ya mji wa Njombe.Kwa halmashauri ya mji Makambako chanjo hiyo itatolewa kituo cha afya Makambako,kituo cha afya cha jeshi 800kj,pamoja na hospitali ya Ikelu.Katika halamsahuri ya Wanging’ombe chanjo itatolewa hospitali ya Ilembula,Kituo cha afya Wanging’ombe pamoja na zahanati  ya Igwachanya \
 
.Kwa upande wa Makete chanjo hiyo itatolewa Makete hospitali,Ikonda hospitali pamoja na hospitali ya Bulongwa.Vile vile katika wilaya ya Ludewa itatolewa hospitali ya Ludewa,Milo hospitali pamoja na Kituo cha afya cha Mlangali.Katika wilaya ya Njombe chanjo inatarajiwa kutolewa kituo cha afya Mtwango,Lupembe na Mtwango.
Mkuu wa mkoa wa Njombe mhandisi Marwa Rubirya akizungumzia juu ya utolewaji wa Chanjo iliyopokewa mkoani Njombe na kutoa rai kwa weananchi kujitokeza ili kupata chanjo hiyo
Baadhi ya viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama wakiwa makini kumsikiliza mkuu wa mkoa wa Njombe wakati akizungumzia suala la chanjo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...