Waziri wa Kilimo Mhe. Prof Adolf Mkenda akikagua ujenzi wa maghala na vihenge vya kisasa vinavyojengwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Kanda ya Makambako leo tarehe 3 Agosti 2021, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Njombe. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Waziri wa Kilimo Mhe. Prof Adolf Mkenda akikagua Skimu ya Umwagiliaji ya Itipingi leo tarehe 3 Agosti 2021, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Njombe.
Waziri wa Kilimo Mhe. Prof Adolf Mkenda akisisitiza jambo wakati akizungumza na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Njombe iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe Marwa Rubirya leo tarehe 3 Agosti 2021, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Njombe.
Waziri wa Kilimo Mhe. Prof Adolf Mkenda akisisitiza akikagua hali ya upatikanaji wa mbolea alipotembelea kwenye ghala la kuhifadhia mbolea la Mtewele General Traders leo tarehe 3 Agosti 2021, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Njombe.
Waziri wa Kilimo Mhe. Prof Adolf Mkenda akisisitiza akisisitiza jambo mara baada ya kukagua ghala la kuhifadhia mbolea la Mtewele General Traders leo tarehe 3 Agosti 2021, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Njombe.

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Iringa

Serikali imeelekeza Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) kununua mahinidi kiasi cha Tani 10,400 zilizohifadhiwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula-NFRA Kanda ya Makambako kwa miaka mitatu mfululizo.

Akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Njombe iliyoanza tarehe 3 Agosti 2021, Waziri wa Kilimo Mhe. Prof Adolf Mkenda amesema kuwa Bodi hiyo imepewa jukumu na serikali la kununua na kuuza nafaka hivyo inapaswa kununua mahindi hayo ambayo yamehifadhiwa katika ubora wa hali ya juu.

Waziri Mkenda amesema kuwa mahindi hayo yaliyohifadhiwa na NFRA yanapswa kuzungushwa/kuuzwa ili kutoa fursa kwa NFRA kuingia sokoni kununua mahindi mengine jambo litakalopelekea wakulima kuwa na ahueni ya soko.

“NFRA ikiingia sokoni itatoa nafasi kwa wakulima watakaouza mahindi yao kuweza kununua pembejeo bora na kulima zaidi mazao ya nafaka” Amekaririwa Waziri Mkenda

Amesema kuwa kazi ya NFRA ni kununua nafaka na kuhifadhi ili ikitokea changamoto yoyote nchini nafaka hiyo iweze kutolewa lakini kwa kuwa hakuna changamoto yoyote iliyojitokeza nchini kwa kipindi cha miaka mitatu hivyo wanapaswa kuyauza ili kununua mahindi mengine kwa ajili ya kuhifadhi.

 Waziri Mkenda amesema kuwa pamoja na mahindi yaliyohifadhiwa kwenye ghala la NFRA Makambako lakini pia kuna Tani 5009.267 za mpunga ambazo pia zinapaswa kutafutiwa masoko hususani ya nje ya nchi.

Akizungumzia kuhusu kusuasua kwa mradi wa ujenzi wa Maghala na Vihenge vya Kisasa Waziri Mkenda amesema kuwa ujenzi huo unafanywa kwa mkopo wa bei nafuu hivyo mkandarasi anapaswa kuhakikisha anamalizia kazi kwa haraka kwa mujibu wa makubaliano.

Katika ziara hiyo ya kikazi ya Waziri wa Kilimo Mhe. Prof Adolf Mkenda kwa siku mbili mkoani Njombe, Waziri Mkenda ametembelea na kukagua ghala la mbolea na Mtewele General Traders, Ghala la YARA, Ghala la ETG, pamoja na kukagua Skimu ya umwagiliaji ya Itipingi.

Waziri Mkenda anatarajiwa kuendelea na ziara ya kikazi katika mkoa wa Songwe na Rukwa kesho tarehe 4 Agosti 2021 na tarehe 5 Agosti 2021.

MWISHO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...