Na Linda Shebby, Kibaha

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge ameahidi kumaliza migogoro ya ardhi katika Mkoa wa Pwani.

RC Kunenge amesema hayo leo alipokuwa akizungumza na Wandishi wa Habari wa Mkoa wa Pwani ambapo alikua ameitisha mkutano huo kwa lengo la kufahamiana na kujiwekea malengo ya mpango kazi Ili kuweza kutangaza Mkoa wa Pwani ndani na nje ya nchi  na rasilimali zake zilizomo.

Aidha amesema Mkoa wa Pwani unachangamoto mbalimbali  ikiwemo upatikanaji wa  habari huku akiahidi milango kuwa wazi na kushirikiana na vyombo mbalimbali Mkoani hapa.

 "Hivi karibuni nitafanya  ziara  ndani ya Mkoa wa Pwani  mimi ni mtawala hivyo nahitaji kutatua changamoto  mbalimbali zinazowakabili wanachi wengi ' alisema Kunenge.
Naye Karibu Tawala Mkoa wa Pwani Mhandisi  Mwanasha Rajab Tumbo alisema kuwa wamewatuma wataalamu mbalimbali katika Wilaya za Bagamoyo na Chalinze ambapo watajihusisha kwa  kung'amua changamoto zinazowakabili wananchi wa na kuzifanyia utatuzi.

"Baada ya kupata mrejesho huo ndipo Mkuu wa Mkoa atakwenda katika  maeneo husika Ili kuweza kufanya utatuzi"
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge akizungumza na Wandishi wa Habari wa Mkoa wa Pwani ambapo alikua ameitisha mkutano huo kwa lengo la kufahamiana na kujiwekea malengo ya mpango kazi Ili kuweza kutangaza Mkoa huo ndani na nje ya nchi  na rasilimali zake zilizomo.
Karibu Tawala Inginia Mwanasha Rajab Tumbo(kulia) na Afisa Habari Zablon Bugingo(kushoto) wakiwa kwenye mkutano huo


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...