Na Mwamvua Mwinyi, Mafia
MWENGE
maalum wa Uhuru ,umepitia miradi 12 yenye thamani ya milioni 95.885
,wilayani Mafia, ambapo agost 18 mwaka huu, utakuwa umehitimisha Safari
yake mkoa wa Pwani tayari kwa ajili ya kukabidhi Dar es salaam .
Akipokea
mwenge huo kutokea Mkuranga ,mkuu wa wilaya ya Mafia ,Mhandisi Martin
Ntemo alisema, kati ya miradi hiyo mmoja umezinduliwa ,kumi imetembelewa
na mmoja kukaguliwa .
Akielezea
mapambano dhidi ya rushwa ,-TAKUKURU wilaya ya Mafia kwa mwaka
2020/2021 imepokea taarifa 30 za vitendo vya rushwa,watu sita
wamekamatwa kwa kuhusishwa na vitendo hivyo .
Ntemo
alifafanua ,tuhuma 15 ziko katika hatua mbalimbali za uchaguzi na
kuokoa milioni 25 .389.322 kutokana na chunguzi mbalimbali.
Pia
alisema ,uongozi wa wilaya na Jeshi la polisi kwa kushirikiana na wadau
pamoja na wananchi wanaendelea na mapambano dhidi ya dawa za kulevya
ambapo hadi Juni 2021 jumla ya kesi 31 zimeripotiwa, huku 28 zikiwa
zimefikishwa mahakamani na 3 bado ziko chini ya upelelezi .
Ntemo alifafanua kwamba, dawa za kulevya zilizokamatwa ni bangi kg.4.2, heroine gram 4.2 na wanaojihusisha na utumiaji ni 34.
Akitoa Ujumbe wa Mwenge , kiongozi wa mbio za mwenge maalum wa Uhuru ,LT.Josephine Mwambashi alikemea matumizi ya madawa ya kulevya na kutaka jamii kuwa washiriki wa kuwafichua wanaojihusisha na madawa ya kulevya na alikemea kupokea na kuomba rushwa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...