NA VICTOR MASANGU,PWANI
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Aboubakari Kunenge katika kukuza sekta ya kilimo
ameamua kufanya ziara ya kuwatembelea baadhi ya wakulima wa zao la
korosho Wilayani mkuranga kwa lengo la kuweza kusikiliza changamoto zao
na kuweka mikakati ya kukuza zao hilo.
Kunenge
katika ziara yake pia ametembelea shamba la Korosho la Mkulima Said
Mbangwi lililopo katika eneo la Mkaliakitumbo kunionea mwenendo mzima
wa maendeleo ya mkulima huyo.
Pia
mkuu huyo wa Mkoa ameweza kufungua vikao vya wadau wa Tasnia ya
Korosho Mkoani Pwani ambapo vitafanyika katika Wilaya tatu za Mkuranga,
Rufiji na Kibiti.
Katika
vikao hivyo vitalenga kuweka Mikakati kabambe ambayo itasaidia katika
kuinua zao la Korosho na kuondoa Changamoto zinazolikabili zao hilo.
Akizungumza
wakati akifungua Mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Flex Garden
Mkuranga Kunenge alimshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais Jamhuri yaMuungano wa Tanzania kwa maelekezo yake ya kuhakisha Wakulima na mazao haya ya biashara yanatuletea tija
Kunenge
alisema kuwa wamekutana kuzungumzia namna kuboresha uzalishaji na
ubora wa Korosho za Pwani. Ameeleza kuwa Mkoa huo mwaka 2018/2019
ulizalisha Tani 23, 266.7 za korosho Mwaka 2020/2021 uzalishaji ulishuka
hadi Tani 7, 0523 na ubora wake ulikuwa wa chini.
Ameeleza
kuwa kushuka uzalishaji kumepekelea Kipato kinachotokana na Korosha
kushuka kutoka Bilioni 31 hadi bilioni 7, "hii haikubaliki, Sisi
Viongozi kama hatuwezi kusimamia zao la Korosho hatuna uhalali wa
kuendelea kuwa kwenye majukumu haya" amesema Kunenge.
"Viongozi
wetu Wakuu wamekwisha sema nini kifanyike, wanataka tuzalishe kwa
wingi, Korosho yetu iwe Bora na impebbei nzuri Mkulima".
Sisi wasaidizi wao tupo kuhakisha uzalishaji na ubora huo unafikiwa" alisema Kunenge.
Aidha
aliongeza kuwa mkulima ambaye amepata fursa ya kunitembelea shambani
kwake amemkuta anakabiliwa na changamoto ya kukosa wataalamu wa zao
hilo.
Mkuu wa mkoa wa Pwani Aboubakari Kunenge wa
katikati akizungumza Jambo wakati alipofanya ziara yake Wilayani
mkuranga kwa ajili ya kuzungumza na wakulima wa zao hilo.
''Wataalamu
wetu wanatakiwa kuto Elimu ya kilimo cha Korosho na kwamba wanatakiwa
wawe wanawatembelea kwa ajili ya kubaini changamoto zao,"alisema
Kunenge.
Pia amewataka Wataalamu wa kilimo na Viongozi Mkoani hapo kubadilika. amewataka kumsaidia mkulima ili kuinua zao hilo.
Kunenge Amewataka wakulima kupalilia mashamba yao na kuachana na tabia ya kupeleka Korosho zenye ubora hafifu kwenye maghala.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...