Na.Vero Ignatus,Arusha.
Mamlaka ya Mawasiliano nchini Kanda ya
kaskazini (TCRA)imeendesha semina ya siku moja, juu ya uzalishaji wa maudhui ya ndani na uzalishaji
wa uboreshaji wa maudui kwa wamiliki wa vituo vya utangazaji mtandaoni (online TV,Bloggers),katika kuzingatia kanuni,maadili,Sheria za nchi pamoja na makosa ya mtandaoni.
Mhandisi Imelda Salum ni Mkuu wa Kanda ya Kaskazini (TCRA)amewataka wamiliki hao wa vyombo vya habari kuwa na ushirikiano, ubunifu ,katika utendaji kazi kwao wa kila siku, kuwa na maudhui chanya yenye mtizamo unaobeba mambo kadhaa wa kadha ,pamoja na kuongeza udadisi katika kujifunza.
Aidha Mhandisi huyo alisema kuwa lengo kubwa la semina hiyo ni kubadilishana uzoefu, kuzijua changamoto mbalimbali ambazo zipo na Kuona namna ambayo watazipatia ufumbuzi,pamoja na kuwakumbusha namna ya kufikiria juu ya kizazi kijacho kutokana na ukuaji wa teknolojia tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Akizungumza mwezeshaji
wa
mafunzo hayo Reuben Boniface ,alisema kuwa lengo kuu la ni kuwakumbusa
kutambua kuwa maudhui ya ndani kwani yana maana pana ,ikiwemo umri,jinsia,mtazamo wa
kiimani,na lugha sahihi inayotumika huku akiwataka kutumia uandishi wa
kuzingatia sheria za nchi bila kuleta mtafaruku.
Aidha Boniface
aliwataka kufahamu kuwa wakati wa kuandaa maudhui ,watambue kwa undani juu ya
yale ambayo yanayoisibu jamii, pamoja na yale ambayo yanawatia hofu,huku wakutambua kazi yao kubwa ni kuelimisha, kuhabarisha pamoja na
kutoa burudani.
Akizungumza mmoja wa mshiriki wa semina hiyo Mussa Juma amesema kuwa kwa kutumia mitandao ina nafasi kubwa ya kutengeneza ajira,kupata fursa mbalimbali,kazi ama biashara kwa mtandao badala ya kukuingiza au kutengeneza maudhui ambayo hayafai kwa jamii
Hivyo amewaasa wamiliki wa vyombo hivyo kuzingatia sheria ,kanuni na bila kusababisha uvunjifu wa amani,huku akisisitiza weledi zaidi unahitajika katika kujenga uelewa mzuri kwa jamii kwa ujumla.
Mwezeshaji Reuben Boniface akizungumza na wamiliki
wa vituo vya utangazaji mtandaoni (online TV,Bloggers) katika semina
ya siku moja iliyofanyika katika hotel ya Golden Rose Jijini Arusha.
Picha zote /habari na Vero Ignatus.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...