Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Chuo cha Ufundi Stadi cha wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya, Agosti 1, 2021. Wengine pichani kutoka kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera, Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako na kulia ni Mbunge wa Busokelo, Atupele Mwakibete. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na aliyekuwa Waziri katika serikali ya Awamu ya Nne, Profesa Mark Mwandosya (kulia) na mkewe Lucy Mwandosya (wa pili kulia) wakati alipowasili kwenye viwanja vya Chuo cha Ufundi cha wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya kuzindua Chuo hicho, Agosti 1, 2021. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Agosti 1, 2021 amekabidhiwa zawadi ya picha aliyopiga akivuka mto Rufiji kwa kutumia ngalawa mwaka 2010 akiwa Mkuu wa wilaya ya Rufiji wakati alipompokea Profesa Mark Mwandosya aliyekuwa ni Waziri katika serikali ya Awamu ya Nne. Picha hiyo ilikabidhiwa kwake na Profesa Mwandosya (kushoto) na mkewe Lucy Mwandosya (wa pili kushoto) baada ya Mheshimiwa Majaliwa kuzindua Chuo cha Ufundi Stadi cha wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya. Wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazma kaunda suti wakati alipotembelea darasa la mafunzo ya ushonaji nguo katika Chuo cha Ufundi Stadi cha wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya, Agosti 1, 2021. Kushoto ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...