Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

MKUU wa Wilaya ya Ikungi Jerry Muro amesema ameona ni busara kuendelea na ziara ya kutoa mrejesho wa kero na changamoto za wananchi ambazo tayari mtangulizi wangu Edward Mpogolo ambaye  kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Same alishaziaikiliza

Akizungunza kuhusu mejesho wa kero,Murro amesema wanachokifanya sio kwenda tena kusikiliza kero bali kupeleka mrejesho wa hatua walizochukua katika kuzitatua zile ambazo tayari mtangulizi mwenzake alishazisikilzia maana Serikali ni taasisi na lazima katika nafasi zao waoneshw uwezo wa taasisi na sio uwezo binafsi wa mtu

"Katika kulitekeleza hili, nimepata fursa ya kuzungumza na wananchi wa kijiji cha kaugeri kata ya Mwaru tarafa ya Sepuka, jimbo la singida magharibi kutoka ikungi mpaka kijiji cha kaugeri kata ya mwaru ni zaidi ya kilometa 350,

"Hapa kulikuwa na changamoto ya umaliziaji wa jengo la Zahanati, nimekwenda sasa kuwapa mrejesho kuwa  Rais, Samia Suluhu Hassan ameridhia Sh.milioni 50 zitolewa na tayari tumeshaingiza kwenye  akaunti ya kijiji kazi inaendelea.

"Hapa tumefanikiwa kutatua kero ya zahanati sasa malengo yetu ni kuboresha zahanati na kuwa na kituo cha afya chenye uwezo wa kuhudumia wananchi wengi zaidi.Rejea maneno ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Hussein Katanga akila kiapo alisema lazima kwenye serikali kuwe na muunganiko wa pamoja (team work) sisi Ikungi tunaitekeleza falsafa hii kwa vitendo sasa,"amesema Murro.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...