Zikiwa zimebaki siku chache darasa la saba kufanya mtihani wao wa Taifa wa kumaliza elimu ya msingi, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Kalist Lazaro amewataka viongozi wa Dini na wazazi kufanya maombi ili Wanafunzi wapate ufaulu mzuri.

Wito huo umetolewa  na Mkuu huyo wa wilaya  wakati wa misa ya shukran ya  Fadher Africanus Kanju  baada ya kusimikwa kuwa Padre wa kanisa katoriki.

  Lazaro alisema  Wilaya ya Lushoto imekuwa haifanyi vizuri katika matokeo ya kila mwaka ya darasa la saba  hivyo alieleza ni muhimu viongozi wa dini wakafanya maombi ili huyo shetani anayefanya watoto wasifanye vizuri asipate nafasi kipindi hiki.

"Nimeangalia takwimu ya matokeo ya kitaifa ya darasa la saba nikakuta shule nane za mwisho zipo katika wilaya yetu ya Lushoto jamani hii ni aibu na fedheha"Alisema  Mkuu huyo wa wilaya.

Alisema kuwa Serikali  inatumia rasilimali kubwa na inatoa elimu bure inapaswa walimu wajitoe katika ufundishaji ili kupatikane  Matokeo mazuri na hatimaye kama wilaya waondokane  katika mnyororo  wa kushika mkia.

Mkuu huyo wa wilaya alisisitiza kuwa katika kupambana na matokeo mazuri wameamua kuanzisha makambi katika shule zote za wilaya hiyo  lengo ni kuongeza ufaulu katika wilaya ya Lushoto kwa ujumla.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...