Na John Walter -Manyara

Kufutia tukio la moto kuteketeza ofisi ya walimu katika shule secondari ya Gichameda iliyopo wilaya ya Babati mkoani Manyara,Jeshi la zimamoto na uokoaji mkoani hapa limeeleza chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme katika jengo hilo.

Akizungumza na kituo hiki Kamishna msaidizi wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Manyara [ACP] Gilbert Mvungi amesema mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa raia mwema kupitia namba ya 114 jeshi hilo lilifika eneo la tukio saa nane na dk 45 mchana.

Aidha ameongeza kuwa moto huo uliunguza ofisi ya walimu na vitabu mbalimbali ambavyo viliteketea, pamoja na ofisi ya fedha huku ya makamu mkuu wa shule ambapo hata hivyo juhudi zilifanyika kuokoa nyaraka zilizpokuwemo katika ofisi hizo.

Sambamba na tukio hilo ACP Mvungi amewataka wakuu wa taasisi za umma na binafsi Mkoani Manyara kuchukua tahadhari ya moto kwa kuweka miundombinu ya kukabiliana na majanga ya moto pindi yanapotokea. Naye mwenyekiti wa kijiji cha Gichameda Alex Joseph amesema alisikia kelele za watu wakiomba msaada ndipo akafika eneo la shule na kujionea tukio hilo la moto na kushirikiana na wananchi wengine wakaendelea kuokoa sehemu ya jengo hilo pamoja na nyaraka na kumbukumbu katika ofisi ya fedha.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo ameeleza kuwa ofisi ya walimu na ofisi ya makamu mkuu wa shule ndizo zilizo athirika na moto huo, licha ya juhudi mbalimbali za kuudhibiti kufanywa na wananchi usiku wa manane.





 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...