Kiwanda cha kutengeneza na kuunganisha magari cha GF Vehicles Assemblers (GFA) kilichopo Kibaha mkoni Pwani kimetoa msaada wa madawati na vitanda kwa watoto yatima wanaolelewa na Taasisi ya elimu ya Wipahs lengo likiwa ni kuwasaidia watoto hao lakini kurudisha sehemu ya faida katika Jamii.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Mkurugenzi wa GFA Imrani Karmali amesema wakati kiwanda hicho kikisherehekea mwaka mmoja tangu kianze kuunda na kuzalisha magari wameona ni vema wakatoa msaada kwa jami

Naye Meneja wipahs, Jabbir Rajan mbali na kushukuru amesema ipo haja kwa taasisi ama kampuni kuiga mfano huo kwa kurudisha sehemu ya faida kwa jamii kwani kwa kufanya hivyo inasaidia kupunguza makali ya kuwahudumia watoto hao.

Meneja mkuu wa kiwanda hicho Ezra Mereng amesema kiwanda kimeendelea kukua na kwa sasa asillimia 95 ya wafanyakazi ni watanzania hii ni baada ya kupewa mafunzo mbalimbali kwa mwaka mzima na watalamu kutoka nchi mbali mbali zenye teknolojia mzuri katika utengenezaji wa Magari,Pia aliongeza kiwanda hicho kipo katika eneo la kibaha hivyo pia kimetoa upendeleo maalumu kwa wakati wa eneo wenye ujuzi ikiwa kama kipaumbele kwao.

Mbali na kutoam misaadfa hiyo kwa wenye mahitaji pia kulifatiwa na tamasha kubwa la michezo ikihusisha wafanyakazi wa kampuni ya GFA pamoja na kampuni mama ya GF Trucks & Equipment katika mpira GFA waliwabugiza wapinzaniao bao 2-0.

Wafanyakazi wa kampuni ya GFA wakiwa wamekaa pamoja na wafanyakazi wao wakati wa kusherehekea mwaka mmoja tangu kuanzishwa na kampuni hiyo inayotengeneza magari iliyopo Kibaha baada ya kukabidhi msaada wa Vitanda ,Madawati na meza kwa tasisi ya Elimu ya WIPAHS kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji wanaosoma katika shule hiyo.
Meneja msimamizi wa tasisi ya Elimu ya WIPAHS Jabbir Rajan akigonganisha mikono na  Wakurugenzi wa kampuni ya kutengeneza na kuunganisha  magari GF  Assembing , Imran Karmal (kulia) kama shukurani na Ali Jawad (kushoto) baada ya kupokea msaada wa vitanda  meza  na viti vya kusomea vilivyotolewa na kampuni hiyo kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji wanaosoma katika shule za tasisi hiyoikiwa ni kutimiza mwaka mmoja toka kuanzishwa kwa kiwanda hicho  kilichopo   Kibaha mkoani  Pwani.


wakiomba dua kabla ya kuanza


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...