Na Mwandisho wetu

Dar es Salaam. Jumla ya klabu tisa (9) ziashiriki katika mashindano ya wazi ya klabu bingwa ya Taifa yalyopangwa  kufanyika kwenye bwawa la kuogelea la klabu ya Gymkhana Septemba 25 na 26.

Klabu hizo  ni, Dar es Salaam Swim Club, Taliss, Champions Rise, Mwanza Swim Club na Arusha Swim Club pia kuna klabu za Mis Piranhas, Bluefins na, FK Blue Marlins kwa kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Chama Cha Kuogelea Tanzania (TSA), Khadija Shebe.

Shebe alisema kuwa mashindano hayo yatashirikisha waogeleaji wenye umri kuanzia miaka tisa (9) na wenye miaka 15 na zaidi katika mashindano hayo yaliyodhaniwa na  Samsa Logistics Limited, Sapphire Court Hotel limited, Selcom Paytech ltd, Pepsi, Azam, Gymkhana Club, Tarmal Industries ltd, Tanpack na Flames Restaurant.

Alisema kuwa kutakuwa na makundi manne, kundi la miaka tisa na 10, 11 mpaka 12, 13-14, na 15 ambapo muogeleaji atakayeibuka wa kwanza atapata pointi 20 ambapo wa pili na tatu watapata pointi 16 na 14 kila mmoja.

“Waogeleaji watakaomaliza katika nafasi ya nne watapata pointi 12 ambapo wa tano, sita, saba, nane, tisa na 10 watazwadiwa pointi 10, 8, 6, 4, 2 na moja. Haya ni mashindano ya TSA na yapo kwenye kalenda ya chama, hivyo waogeleaji wenye vigezo wanatakiwa kushiriki katika mashindano haya,” alisema.

Alisema kuwa jumla ya staili tano za kuogelea zitashindaniwa katika mashindano hayo ambazo ni backstrokes, butterflies, individual medleys, breaststrokes na freestyles.

“Tunawashukuru wadhamini ambao mpaka sasa wamejitokeza kusaidia mashindano haya. Wametupa faraja na moyo wa kuendeleza mchezo huo, bado tunaomba wadhamini wajitokeze kudhamini mashindano haya. Ni mashindano ya kupima vipaji vya waogeaji wetu ambao wataiwakilisha nchi katika mashindano haya,” alisema Shebe.

Waogeleaji wakijaindaa kushindana kwenye  mashindano ya wazi ya taifa ya yaliyopangwa kufanyika kwenye bwawa la kuogelea la klabu ya Gymkhana Septemba 25 na 26.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mwandishi kabla ya kuposti asahihishe kasoro za maneno.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...