Na Zainab Nyamka, Michuzi TV
UONGOZI wa klabu ya Kinondoni Municipal Council (KMC) kimetangaza kikosi cha wachezaji 29 kitachoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa 2021/22.
Taarifa hiyo iliyotolewa na Afisa Habari na Mawasiliano wa KMC Christina Mwagala imesema kikosi hicho ndicho kitachokuwa kikicheza kwenye msimu wa Ligi Kuu unaotarajia kuanza Septemba 27 mwaka huu.
Benchi la ufundi kwa Msimu wa 2021/22 litasimamiwa na Kocha Mkuu John Simkoko, Kocha Msaidizi ni Habibu Kondo na Hamad Ally, Kocha wa Magolikipa ni Fatuma Omary
Kikosi hicho kimekuwa na maingizo mapya na wengine wakisajiliwa na timu zingine na kwa upande wani Golikipa mkongwe Juma Kaseja na Farouk Shikalo akijiunga na timu hiyo akitokea Yanga, Denis Richard na Sudi Dondola.
Walinzi ni Andrew Vicent Chikupe, Ismail Adam Gambo, Mohamed Kassim, Abdulrazack Mohamed, Kelvin Kijiri, Hassan Khamis Ramadhan, Ally Ramadhan na Nickson Clement Kibabage
Kwa upande wa Eneo la kati, KMC watapata huduma kutoka kwa Jean Baptiste Mugiraneza, Masoud Abdallah Kabaye, Mohamed Samatta, Kenny Ally Mwambungu, Awesu Awesu, Abdul Hillary, Hassan Salum Kabunda, Iddi Kipagwile, Miraji Athuman, Martin Kigi ma Emmanuel Mvuyekure
Washambuliaji ni Matheo Anthony, Sadalla Lipangile, Charles Ilamfia, Nassor Saadun, Hassan Kapalata na Clif Buyoya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...