Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi  George Simbachawene, ametoa maelekeza kwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama nchini kuwatafuta watu wote wanaowachafua wenzao mitandaoni hasa wanaomdhihaki Rais wa Tanzania na Serikali na hatua kali zifuatwe na kuwafikisha mahakamani kwa haraka.

Ametoa maelekezo hayo leo Septemba 16,2021 Mjini Dodoma wakati akizungimza na viongozi wa idara zote za ulinzi na usalama nchini ambapo ameelekeza kufanyike msako wa haraka kuwabaini watu hao na kuwakamata.

"Kumeibuka  tabia ya watu kutumia vibaya mitandaoni ya kijamii kwa kisingizio cha uhuru wa kujieleza,"amesema Waziri Simbachawene huku akisisitiza msako wa kubaini watu hao uanze haraka na kisha sheria ichukue mkondo wake.

Katika hatua nyingine Waziri Simbachawene ameagiza msako wa wezi mitandaoni kwa kuwa inakadiriwa kuwa kwa siku milioni 500 zinakua kwenye wizi wa kimatandao huku akikataza wananchi kutoa fedha kwa ajili yakufuatilia Polisi taarifa za simu zao zilizoibiwa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...