Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo


MAMLAKA  ya Udhibiti Ununuzi wa Umma PPRA  imetoa mafunzo kwa wakuu wa vitengo vya manunuzi na ugavi 900 wa Halmashauri hapa nchini ili kupata uelewa zaidi juu ya masuala hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari wilayani Bagamoyo ,wakati wa mafunzo juu ya taratibu sheria na kanuni za manunuzi ya umma ,Frank Yesaya ofisa manunuzi na ugavi ,alisema mafunzo hayo yalitolewa kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Pia aliwataka maofisa hao kufuata Sheria za manunuzi ili kuepukana na  hoja  ambazo zinaweza kujitokeza wakati ukaguzi wa mikataba ya  miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa katika halmashaurli  hizo.

Awali akifungua mafunzo hayo katibu tawala wa mkoa wa Pwani , Mwanasha Tumbo aliwataka maofisa hao kusimamia manunuzi na mikataba mbalimbali ya miradi ya maendeleo ili iweze kuleta manufaa kwa wananchi.

Ismail Kiwela mwenyekiti wa halmashauri Chalinze,alishukuru kupata uelewa juu ya masuala ya manunuzi na namna halmashauri inavyotoa tenda na kutafuta mawakala ili kutekeleza masuala ya maendeleo.

Alisema, ni jukumu lao kuwa mabalozi wa kwenda kusimamia manunuzi na mikataba inayotolewa.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...