- Asema Magari mabovu na Gereji bubu kwenye maeneo ya road reserve ni chanzo Cha uchafuzi wa mazingira.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amewaelekeza watu wote walioegesha Magari mabovu kwenye hifadhi ya Barabara katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo ikiwemo Tandale ambalo limekithiri kwa changamoto hiyo kuanza maandalizi ya kutaondoa.

RC Makalla ametoa katazo hilo wakati wa Mwendelezo wa ziara ya kusikiliza na kutatua Migogoro ya Wananchi ambapo Leo ilikuwa zamu ya Wananchi wa Jimbo la Kinondoni kupaza sauti zao.

Aidha RC Makalla amesema kumeibuka tabia ya watu kuyahifadhi magari mabovu Barabarani na kusababisha Uchafu wa mazingira pamoja na kuziba eneo la Barabara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...