Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
MTAA
wa Muheza,Kata ya Mailmoja ,Kibaha ,mkoani Pwani ,inatarajia kuhesabu
watu na makazi katika zoezi la sensa ya majaribio ,itakayofanyika siku
tatu kuanzia tarehe 10 usiku wa kuamkia tarehe 11 September hadi 13
,Mwaka huu.
Akielezea
kuhusiana na utekelezaji ya sensa ya majaribio ,wakati wa kikao Cha
kamati ya sensa ,mratibu wa sensa wilaya ,Wambura Yamo alieleza ,kwa
mwaka 2021 serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendesha sensa
hiyo ya majaribio katika mikoa kumi na moja Tanzania Bara, na miwili
Zanzibar.
Alisema ,imeanzwa kutekelezwa katika maeneo husika kuanzia septemba 8 hadi September 19 mwaka huu.
"Mkoa
wa Pwani ikiwa ni iyoteuliwa miongoni mwa mikoa 11 Tanzania Bara
iliyoteuliwa kufanyia sensa ya majaribio katika kata ya Muheza
"alifafanua Wambura.
Aidha
alibainisha ,kuanzia septemba 8 hadi 10 ni siku tatu ambazo makarani
watatambua ramani ya eneo la kuhesabia a huduma za jamii ikiwemo
shule,vyanzo vya maji,vituo vya afya,zahanati ,maduka ya dawa,kaya za
jumuiya kama magereza ,vituo vya kulelea wazee na watoto ,kambi za
wavuvi na wasio na makazi maalum ,wasafiri.
Wambura aliweka bayana ,tarehe 14 September hadi 16 September mwaka huu itahusu makarani kuhesabu nyumba na majengo.
"Tarehe 17 September hadi 19 September mwaka huu itahusu makarani kuhesabu anuani ya makazi"
Wambura
alisema ,sensa hiyo inafanyika ili kufanikisha ubora na ufanisi wa
vitendea kazi yenye teknolojia mpya itakayotumika kwenye sensa ya watu
na makazi ya mwaka 2022 agost 28.
Nae
mkuu wa wilaya ya Kibaha , Sara Msafiri alieleza, serikali inatumia
fedha nyingi kutekelezwa zoezi hili muhimu hivyo wananchi hao
wasiiangushe wilaya .
Msafiri alisema,anaamini watafanya vizuri na kuwa mfano wa kuigwa na kuongeza'" ametaka walengwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo ili majaribio yaleta matokeo chanya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...