Na Zainab Nyamka, Michuzi TV

BODI ya Ligi (TPLB) imetangaza ratiba ya Ligi Kuu Tanzanua Bara itakayoanza kutimua vumbi Septemba 27 mwaka huu.

Bodi ya Ligi wameweka wazi ratiba hiyo ambapo watani wa jadi Simba na Yanga Zitakutana tena Desemba 11 ukiwa ni mchezo wa tano ndani ya mwaka mmoja.

Timu hizo tayari zimekutana mara tatu na  zinatarajia kucheza kwenye mchezo wa Ngao ya Hisani Septemba 25 ukiwa ni mchezo wa nne ndani ya mwaka mmoja.

Yanga na Simba zimekutana kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la Mapinduzi ambapo Yanga walifanikiwa kushinda kwa mikwaju ya penati, wakakutana tena kwenye mchezo wa ligi kuu Yanga ikiibuka kwa ushindi wa goli 1-0.

Mchezo wa tatu ulikua ni wa Fainali ya Kombe la Azam, Simba waliibuka kidedea kwa kushinda Na kuqa mabingwa wa kombe hilo.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...