Na Joseph Lyimo
UKATILI
wa kijinsia unakinzana na haki za binadamu, utu wa mtu unapashwa
kudhamini kwani kila mtu ni sawa chini ya sheria haijalishi ni mwanaume,
mwanamke au mtoto.
Matukio
ya ukatili wa kijinsia mkoani Manyara, yamekuwa yakitokea mara kwa mara
kwa vyombo vya habari kuripoti ikiwemo vipigo kwa wanawake na watoto
hadi kusababisha majeruha au vifo.
Jeshi
la polisi mkoani Manyara, kupitia dawati la jinsia wamekuwa wakitoa
elimu kwa jamii kutochukua sheria mkononi na kushirikisha vyombo vya
sheria lakini suala hilo llimekuwa bado halijawaingia watu ipasavyo
kwani matukio ya ukatili kwa wanawake na watoto bado yanaripotiwa
kutokea.
Kamanda wa
polisi wa mkoa wa Manyara, kamishna msaidizi (ACP) Merrison Mwakyoma
amesema matukio ya ukatili wa kijinsia yamekuwa yakitokea mara kwa mara
japokuwa wamekuwa wakitoa elimu kwa jamii ili kukomesha hayo.
Kamanda
Mwakyoma amesema hivi karibuni kulitokea matukio zaidi ya 10 ya
ukiukwaji wa haki za binadamu ambapo wanawake na watoto walifanyiwa na
watuhumiwa wanashikiliwa polisi au kufikisha mahakamani.
Ametaja
baadhi ya matukio hayo ni Agosti 19 mwaka huu kwenye mtaa wa Silaloda
mjini Mbulu, Harold Hhando (35) alimuua mtoto wa kike wa kaka yake
Emmanuela Hhando (13) na kumpasua katikati ya miguu na kumtenganisha
vipande viwili na kutoa maini ili ayapike.
Amesema
Agosti 23 mwaka huu mkazi wa kijiji cha Kiongozi wilayani Babati Lucas
Mangu (46) alimuua kwa kipigo mke wake Anna Kisino (41) kwa wivu wa
kimapenzi hata hivyo naye Mangu alijinyonga.
“Tukio
lingine la ukatili kwa mtoto lilitokea Septemba 12 mwaka huu mjini
Babati ambapo Janeth Vicent alimchoma moto sehemu mbalimbali za mwili
motto wake wa miaka mitatu baada ya kumuomba fedha mpita njia,” amesema
kamanda Mwakyoma.
Amesema
Septemba 4 mwaka huu kinyozi wa mji mdogo wa Mirerani wilayani
Simanjiro, Athuman Rajabu (57) alimlawiti mvulana mwenye umri wa mika 16
ambaye ni mlemavu wa kusikia na kuzungumza.
Mkazi
wa Dagailoi mjini Babati, John Paulo amesema matukio ya wanaume kupiga
au kuwaua wanawake kutokana na wivu wa kimapenzi yamekuwa yakijirudia
mara kwa mara.
Paulo
amesema ni bora kumuacha mwanamke kuliko kumpiga au kumsababishia kifo
kwa wivu wa mapenzi ambayo mara nyingi inakuwa hakuna uhalisia ni kuhisi
tuu na kuchukua hatua kali.
Mratibu
wa chama cha wanasheria wanawake Tanzania (TAWLA) kanda ya kaskazini,
mwanasheria Happiness Mfinanga amesema jamii haipaswi kufumbia macho
ukatili ila wanapaswa kutoa taarifa kwa vyombo husika.
“Jamii
ipaze sauti kwenye hilo kwani kuna vyombo vya kisheria ambavyo
vinawaelekeza kutoa ushauri ili kuepuka madhara zaidi ya ukatili
majumbani mwetu,” amesema Mfinanga.
Amesema
vipo vyombo vya kutoa taarifa ikiwemo dawati la jinsia ili kuepusha
matukio ya kikatili yanayotokea kwa jamii siyo ya kufumbia macho na
ushirikiano uanze kwenye familia hadi serikalini.
Mwandishi
wa habari mwandamizi Peter Saramba anasema kwa mtazamo wake, tatizo la
mwanaume kumuua mwanamke kutokana na wivu wa mapenzi ni ukatili wa
mmomonyoķo wa maadili kuanzia kwenye kuanzisha mahusiano na hata kuishi
kwenye mahusiano yenyewe.
Saramba
anaeleza kuwa watu wanaingia kwenye mahusiano na hata kufikia hatua ya
ndoa bila kila mmoja kumfahamu vema mwenzake na baadhi ya walioko kwenye
mahusiano wanataka waendelee kuishi maisha yao ya mwanzo kabla ya
uhusiano.
“Jambo ambalo
kiuhalisia haiwezekani kwa sababu mahusiano na ndoa ni jela ya hiari
anakoingia mtu akifahamu vema kuwa anajifunga kwa mwingine, ni kwa
sababu yeyote anayeingia jela lazima apoteze baadhi ya vitu au mambo
anayoyapenda lakini hayaruhusiwi jela,” amesema.
Amesema
watu wengi waliopo kwenye mahusiano na ndoa hawazungumzi kujadili na
kutafutia ufumbuzi matatizo na changamoto zao na wanawake hutumia silaha
na mbinu za kike, hivyo hivyo wanaume kwao pia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...