Mkurugenzi wa Tamasha la Marafiki Isack Kabeneko(wa kwanza kulia) akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) katika ukumbi wa Kituo cha Utamadini cha Alliance Francaise jijini Dar es Salaam wakati akitangaza tamasha la Marafiki linalotarajia kuanza Oktoba 7 hadi Oktoba 10 mwaka huu.Wapili kulia ni Soumeya Djaffar kutoka Ubalozi wa Ufaransa nchini Tanzania na watatu kulia ni Mkurugenzi wa Bedja Music Nuri Bejda.
Mwakilishi kutoka Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA) Ibrahim Ibengwe (wa kwanza kulia) akizungumzia umuhimu wa tamasha hilo la Marafiki pamoja na kutoa pongezi kwa wadau wote ambao wamekuwa wakishiriki kikamilifu kuendeleza sekta ya sanaa nchini.
Mkurugenzi wa Bedja Music Nuri Bejda(wa kwanza kushoto) akifafanua jambo leo Oktoba 5,2021 jijini Dar es Salaam wakati wa kutangazwa kwa tamasha la Marafiki linalotafrajia kufanyika Oktoba 7 hadi Oktoba 10 mwaka huu.Wapili kushoto ni Soumeya Djaffar kutoka Ubalozi wa Ufaransa nchini Tanzania na watatu kushoto ni Mkurugenzi wa Tamasha la Marafiki Isack Kabeneko.
Mwanamuziki kutoka nchini Kenya Akothe Jumadi(kushoto) na Nuri Bedja wakitoa kionjo cha burudani kwa waandishi wa habari na wadau wa sanaa waliohudhuria mkutano wa kuzungumzia tamasha la Marafiki linalotarajia kufanyika Oktoba 7 hadi Oktoba 10 mwaka huu.
Mkurugenzi wa Tamasha la Marafiki Isack Kabeneko(kushoto) akisisitiza jambo kwa waandishi.Kulia ni Mwakilishi kutoka BASATA.
Mwakilishi kutoka BASATA Ibrahim Ibengwe(wa pili kulia) akielezea namna ambavyo wamekuwa wakishirikiana na wadau wa sekta ya sanaa nchini katika kuhakikisha matamasha yanayofanyika yanakidhi viwango.
Soumeya Djaffar kutoka Ubalozi wa Ufaransa nchini Tanzania(katikati)akizungumzia namna ambavyo Ubalozi huo unavyoshirikiana na wadau wa sanaa nchini kukuza na kuendeleza vipaji vya wasanii.
Mwanamuziki kutoka nchini Kenya Akothe Jumadi(kushoto) na Nuri Bedja wakipongezana baada ya kutoa burudani kwa waandishi na wadau wa sanaa nchini.
Mkurugenzi wa Tamasha la Marafiki Isack Kabeneko(watatu kulia) akitangaza bei ya tiketi ambazo zitatumika kuingia kwenye tamasha la Marafiki.
Mwakilishi kutoka BASATA Ibrahim Ibengwe(wa kwanza kulia) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari.


Na Said Mwishehe, Michuzi TV 

KITUO cha Utamaduni cha Alliance Francaise jijini Dar es Salaam kwa kushirikana na wadau wengine kinatarajia kuwakutanisha wasanii zaidi ya 128 kupitia tamasha la Marafiki linatarajia kuanza Oktoba 7 hadi 10,2021.

 Kwa mujibu wa ratiba , Oktoba 7 na Oktoba 8 litafanyika Nafasi Art Space Mikocheni, Oktoba 9 litafanyika Kituo cha  Alliance Francaise ambacho kipo chini ya Ubalozi wa Ufaransa nchini Tanzania na Oktoba 10 tamasha litafanyika Firefly -Bagamoyo.

Akizungumza wakati kutangaza tamasha hilo leo Oktoba 5,2021 ,Mkurugenzi wa Alliance Frabcaise Flora Valleur amesema Marafiki ni tamasha la muziki la kimataifa ambalo huwaleta wasanii wa ndani na wa nje kuonesha umahiri wao katika eneo la sanaa ya muziki.

"Tamasha hili linaleta wadau na watalaam wa sanaa  kushiriki pamoja na kubadilishana uzoefu na maarifa kwa lengo la kuwajengea uwezo wasanii katika maeneo mbalimbali ya sanaa.Tamasha la Marafiki linatarajia kuleta muziki mzuri wa moja wa moja na maarifa wakati mmoja kuanzia Oktoba 7 hadi Oktoba 9,'amesema Valleur.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tamasha la Marafiki, Isack Kabeneko amesema  wametangaza rasmi tarehe za kufanyika kwa tamasha hilo na tiketi zitanza kuuzwa mapema kwa Sh.10,000 na watakaonunua mlango Sh.15,000.Tiketi zinapatikana Nafasi Art Space -Mikocheni, Firefly -Bagamoyo na Alliance Francaise-Dar es Salaam,"amesema.

Akifafanua kuhusu tamasha hilo amesema kauli mbiu ya mwaka hii inasema "Muziki ni kwa maendeleo ya kijamii", hivyo wamejikita kuhamasisha vijana ambao wamejiajiri kupitia sanaa kutengeneza tungo zenye tija na maudhui kwa jamii na kugusia maeneo tofauti tofauti.

"Katika tamasha la Marafiki tutakuwa na wasanii 128, bendi 16 na wote watatumbuiza wakati wote wa tamasha likiendelea katika maeneo ambayo tumetaja, wasanii wataonesha vipaji vyao katika kuimba na sanaa nyingine tofauti tofauti.Kwa kutambua ukubwa wa tamasha hilo mbali  ya wasanii kuonesha umahiri wao katika eneo la sanaa.

"Tutakuwa na semina za mafunzo na mijadala ya wazi, lengo ni kundeleza sekta ya sanaa kwa kuweka mipango ambayo tunaamini wasanii watanufaika kupitia sanaa wanayoifanya.Mafunzo yatajikita kuwajengea uwezo wasanii,"amesema.

Amefafanua wanataka kuona jamii ya wasanii yenye maendeleo , yenye tija na kunufaika kupitia sanaa huku akieleza kuwa kupitia tamasha hilo wanawake watakuwa na fursa ya kupaza sauti zao kuelezea wanachotaka ili mambo yaende.

Kwa upande wake Ibrahim Ibengwe kutoka Baraza la Sanaa  Tanzania(BASATA) amesema  baraza hilo linafurahishwa na jitihada ambazo zinachukuliwa na wadau wa sanaa katika kuendeleza sekta hiyo.Hivyo wamekuwa wakiunga mkono wadau wote ambao wanaweka mikakati ya kuiendeleza sekta ya sanaa nchini.

"BASATA tumekuja hapa Alliance Francaise kwa ajili ya kuwaunga mkono wadau wetu muhimu katika sekta ya sanaa nchini kwa maana ya wandaaji wa matukio mbalimbali ya sanaa, hivyo Marafiki  Festival ni miongoni mwa matukio yanayoratibiwa na baraza letu.

"Kwa hiyo tunaendelea kutekeleza juhudi za Serikali kwa kuhakikisha shughuli za sanaa hasa matamasha yanafanyika kwa ubora stahiki, kuna vigezo ambavyo BASATA  tunavizingatia kuhakikisha matukio haya yanafanyika kwa taratibu unaoeleweka ili yawe na tija kwa Serikali, wasanii na waandaaji,"amesema Ibengwe.

Ameongeza lengo la matamasha hayo ni kutengeneza mazingira rafiki na kutoa fursa kwa wadau wa sanaa, kwa maana wasanii wa aina zote kuonesha kazi zao kupitia tukio hilo na wanapozionesha watalipwa, hivyo wataogeza kipato.Pia kutakuwa na shughuli nyingine za kijamii ambazo kupitia shughuli hizo jamii nayo itapata fedha.

Baadhi ya wasanii watakaoshiriki kwenye tamasha hilo ni Akoth Jumadi, Bahati Female Band, Balaa MC,Dabo Mtanzania, Iju Music, Justine Kaozya, Kudra Mazongela, Nasibo Mutize, Sinaubi Zawose na Stone Town Rockerz.

Wengine ni  Tarajazz  Zanzibar, Tofa Boy, Voice Revolution Band, Witiri Ubuntu na  Ziad Daroueche.Tamasha litakuwa linaanza saa 12 jioni hadi saa sita usiku wakati semina ya mafunzo na mijadala itakuwa inafanyia kuanzia saa nne asubuhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...