Benki ya Exim imezindua kampeniya ‘Weka Mkwanja Tukutoe!’inayolenga kuhamasisha watanzania kujiwekea amana huku wakipata fursa za kunyakua zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu pamoja na gari aina Toyota Vanguard.

Kampeni hiyoya miezi mitatu inayofahamika kama ‘Weka mkwanjatukutoe!’ imezinduliwa leo jijini Dar es Salaam na imepangwa kuwafikia watanzania wote wakiwemo wateja wa benki hiyo pamoja na wale watarajiwa.

Akizungumza wakati hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo jijini Dar es Salaam leo, Mkuu wa Huduma ya wateja Rejareja na wajasiriamali wa Benki ya Exim, Bwana Andrew Lyimo alisema kampeni hiyo inalenga kuleta mabadiliko kwenye mtazamo wa uhifadhi wa amana miongoni mwa watanzania kutoka kuhifadhi pesa majumbani na badala yake wazihifadhi kupitia benki hiyo kwa usalama wa fedha zao sambamba na faida nyingine nyingi ikiwemo riba.

“Lengo si tu kuhamasisha watanzania kujenga utamaduni wa kujiwekea amana, tunachohitaji ni kuona kwamba Watanzania wengi wanajiwekea amana zao sehemu salama ili kujiendeleza kukua kiuchumi ndio maana tumejipanga kuwahamasisha watumie akaunti zetu mbalimbali ikiwemo akaunti ya mshahara inayotumika kwa matumizi mbalimbali ya kila siku,’’

“Nyingine ni akaunti ya mzalendo inaendeshwa bila makato ya kila mwezi, akaunti ya haba na haba, akaunti ya faida hizi zinakuruhusu kuweka akiba na kupata riba, tuna akaunti ya Nyota ambayo ni akaunti maalum kwa ajili ya kuwawekea Watoto akiba ya badae na mwisho kabisa tuna akaunti ya wajasiriamaliinayowahudumia wafanyabiashara na mahitaji yao tofauti tofauti ya kibiashara ’’ alisema Bw. Lyimo.

Akitaja zawadi zikazotolewa kupitia akaunti hiyo, Bw. Lyimo alisema ni pamoja na zawadi za fedha taslimu kiasi cha Tsh. milioni 1, kwa mwezi na kila mwezi kutakua na washindi sita, sambamba na kuingia kwenye droo itakayowawezesha kushinda zawadi kubwa ya gari aina ya Toyota Vanguard.

“Hivyo basi wateja wetu wa sasa na wale wapya watakuwa kwenye nafasi ya kujishindia zawadi hizi kila wakapojiwekea akiba ya kuanzi Tsh. 500,000 na kuendelea. Kadili wanavyojiwekea amana kubwa zaidi ndivyo wanavyojiweka kwenye nafasi ya kushinda zawadi kubwa zaidi,’’ alisema.

Mkuu wa Huduma ya wateja Rejareja na wajasiriamali  wa Benki ya Exim, Bwana Andrew Lyimo (katikati) sambamba na wafanyakazi wengine wa benki hiyo wakionesha ufunguo wa gari aina ya Toyota Vanguard (inayoonekana nyuma) itakayotolewa kwa mshindi wa kampeni mpya ya benki hiyo inayofahamika Weka Mkwanja Tukutoe!’inayolenga kuhamasisha watanzania kujiwekea amana wakati wa hafla fupi ya unzinduzi wa kampeni hiyo jijini Dar es Salaam jana.

wafanyakazi wa benki ya Exim wakionesha gari aina ya Toyota Vanguard itakayotolewa kwa mshindi wa kampeni mpya ya benki hiyo inayofahamika Weka Mkwanja Tukutoe!’inayolenga kuhamasisha watanzania kujiwekea amana wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa kampeni hiyo jijini Dar es Salaam jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...