Na Khadija Kalili, Kibaha 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linamshikilia mtu mmoja  Abdul Selemani  (27), kabila  Mluguru mfanyabiashara ya Stationary mkazi wa Visiga kwa kipofu, Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani kwa kosa kutengeneza nyara za Serikali. 

Akizungumza na Waandishi wa habari Leo Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani RPC  Wankyo Nyigesa alisema  kuwa  tarehe 12.10.2021 majira ya saa 11:38 jioni katika  eneo la Visiga kwa Kipofu Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola walimkamata  mtuhumiwa  huyo  kwa kosa la kutengeneza na kuuza vitambulisho vya Taifa vya NIDA na kuviuza Tsh 10,000/- kwa kila kitambulisho kimoja  anachotengeneza.
RPC  Wankyo alivitaja vifaa mbalimbali alivyokuwa anatumia kuwa ni Vitambulisho viwili vya Taifa vya NIDA, komputa mpakato, Pvc card, Desktop Computer, Monitor, Frash Disk na Printer. 

Aidha mtuhumiwa huyo  atafikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Wakati huohuo alimtaja mtuhumiwa mwingine anyedauwa kutapeli  watu mbalimbali  aliyemtaja kwa jina la Peter  Baziro ambaye pia hutumia  la Pius  Jaulos Nducha  alikamatwa  14/10/2021 majira ya saa 10:00 jioni huko kwa mfipa, Wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani, Peter  kwa kuwatapeli watu mbalimbali kwa kuwauzia viwanja na kughushi hati za viwanja anavyoviuza na hati za mauzo.

"Pia amekuwa akitapeli watu na kujipatia fedha kwa kuwauzia magari, mpaka anakamatwa  amejipatia pesa kutoka kwa watu mbalimbali akiwemo Bi Jenifa Asa aliyemlipa mtuhumiwa  kiasi cha Mil.4  kwa lengo la kumuuzia eneo  la ukubwa wa 20 kwa 20 huku akijua kwamba siyo
 kweli na hana eneo hilo. 

RPC  Wankyo alisema kuwa mtuhumiwa huyu amekuwa akibadilisha majina kila anapofanya tukio la kutapeli mtu ili asikamatwe. Baada ya mahojiano mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.
Alisema kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linaomba mtu yeyote aliyewahi kutapeliwa na mtu huyu afike kituo cha Polisi kibaha mji kwa utambuzi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...