Ubalozi wa Tanzania nchini Namibia umeandaa maonyesho ya biashara yanayofanyika kuanzia tarehe 4 hadi 8 Oktoba, 2021 katika Kituo cha Biashara cha Wernhil (Wernhil Shopping Mall) kilichopo mjini Windhoek. Maonesho haya muhimu katika utelezaji wa Diplomasia ya Uchumi yanalenga kutangaza bidhaa za Tanzania na Utalii nchini humo ili kukuza biashara na kuvutia wawekezaji nchini.

Katika maonesho hayo Ubalozi umewashirikisha Watanzania wajisiriamali na wafanyabiashara waishio nchini humo (diaspora) ambao wamejitokeza kuonesha bidhaa mbalimbali ikiwemo mchele, korosho, kahawa, asali, majani ya chai, maharagwe, vitenge, batiki na nguo za kufuma.

Sambamba na kunesha bidhaa maonyesho haya yamejumuisha uuzaji wa vyakula mbalimbali vya kitanzania ambavyo vimekuwa vivutio kwa wateja wengi.

Maonesho hayo yalifunguliwa na Balozi wa Tanzania nchini Namibia Mhe. Dkt. Modestus Kipilimba tarehe 4 Oktoba 2020.


Balozi wa Tanzania nchini Namibia Mhe. Dkt. Modestus Kipilimba akiwasili katika Kituo cha Biashara cha Wernhil (Wernhil Shopping Mall) kilichopo mjini Windhoek, Namibia kwa ajili ya ufunguzi wa maonesho ya biashara.


Balozi wa Tanzania nchini Namibia Mhe. Dkt. Modestus Kipilimba akitazama sehemu ya bidhaa za Kitanzania kwenye maonesho yanayoendelea katika Kituo cha Biashara cha Wernhil Shopping Mall mjini Windhoek, Nambia.

Balozi wa Tanzania nchini Namibia Mhe. Dkt. Modestus Kipilimba akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wafanyabiashara wa Kitanzania waliojitokeza kuonesha bidhaa zao kwenye maonesho yanayoendelea katika Kituo cha Biashara cha Wernhil Shopping Mall mjini Windhoek, Namibia.

Sehemu ya wafanyabiashara wa Kitanzania wakionesha bidhaa zao kwenye maonesho yanayoendelea katika Kituo cha Biashara cha Wernhil Shopping Mall mjini Windhoek, Namibia.

Balozi wa Tanzania nchini Namibia Mhe. Dkt. Modestus Kipilimba akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Ubalozi huo walipotembele maonesho ya Biashara yanayoendelea katika Kituo cha Biashara cha Wernhil Shopping Mall mjini Windhoek, Namibia. 

 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...