Na Mwamvua Mwinyi, Mkuranga
MBUNGE
 wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega amewahakikishia wakazi wa 
KondoMwelanzi kata ya Bupu kupata kipaombele Cha kujengewa daraja la mto
 Kipilimba ili kuondoa kero wanayoipata wakati wa mvua kushindwa 
kupitika.
Aidha mbunge 
huyo ameielekeza wakala wa barabara Vijijini (TARURA )wilaya ya Mkuranga
 kuzipa kipaombele barabara kero Kibudi- Mbulani pamoja na Panzuo shule 
ambapo wakazi wa Kibudi hulazimika kutumia usafiri wa pikipiki kwenda na
 kurudi sh.10,000.
Ulega 
alibainisha hayo katika ziara yake ya Jimbo kata ya Panzuo na Bupu 
kwenye vijiji vya Mbulani,Tundu,Kibudi,na Kondo Mwelanzi ambapo aliitaka
 TARURA kuweka ujenzi wa daraja hilo katika bajeti ijayo 2022-2023.
Alieleza
 ,imeshatolewa milioni 100 kwaajili ya maboresho barabara kuu ya Bupu 
-Kiparanganda sasa TARURA ifungue na barabara Tundu-Kiziko ,Bupu-Kibudi 
,Zogowale kuondoa eneo korofi,ili kuleta maendeleo kwa wananchi.
Ulega aliielekeza pia TANESCO 
kufikisha
 umeme Mbulani-Panzuo kwa wateja walikwishalipia ,zahanati ya 
Panzuo,sekondari Panzuo,na Shule ya sek Mandikongo na Shule ya msingi 
Mamrimpera.
Aliwaeleza wananchi wa kata hizo kuvuta subira kwa changamoto ambazo bado zipo kwenye mchakato wa kutatuliwa.
"Serikali
 ya awamu ya sita inapiga kazi katika sekta zote ,na hadi sasa mh.Rais 
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan ameshatoa tilioni
 1.3 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 15,000 nchi nzima,
"Serikali pia imetenga kiasi cha sh.bilioni 966 kwa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) ili kuboresha barabara pamoja na madaraja maeneo mbalimbali nchini"Yaani Samia anaupiga mwingi ile mbaya ,tumpe ushirikiano na tuendelee kumuamini na kumuunga mkono"alisisitiza Ulega.
Katika
 ziara hiyo Ulega ametoa mifuko ya saruji 50 na sh.500,000 katika ujenzi
 wa zahanati Kibudi na pamoja na mifuko ya saruji 50 na sh .500,000 Bupu
 ujenzi wa zahanati ,500,000 ujenzi wa msikiti ,Tundu ujenzi wa nyumba 
ya mganga 500,000 na mifuko ya saruji 50,Mbulani mifuko ya saruji 50 na 
sh .400,000 kwa ajili ya wodi ya wazazi zahanati ya Mbulani na 
amechangia baadhi ya vikundi vya akinamama ikiwa ni fedha sh 800,000 
fedha zake binafsi.
Awali
 diwani wa kata ya Panzuo Dude Hamis alisema, wanakabiliwa na changamoto
 ya umeme ambapo nyumba zilizokadiria zilikuwa 125 zilizopata ni 20 
pekee licha ya wateja hao kulipia toka Juni mwaka huu huku zahanati 
wakitumia tochi na vibatari.
Jingine
 ni shule ya msingi ni ya muda mrefu imejengwa miaka ya 70 ,hawajapata 
madarasa na yaliyopo ni chakavu , barabara ya Zogowale ni eneo korofi 
eneo la mlima linahitajika kujengwa mitalo .
Meneja wa TARURA Mkuranga Silas alisema tayari kiasi Cha sh .milioni 120 kipo kwa ajili ya bajeti hii .
Akijibu kuhusiana na ombi la ujenzi wa daraja Dondwe-mto Kipilimba alisema amelipokea na watalipa kipaombele bajeti ijayo .
Nae
 meneja wa TANESCO Mkuranga Theodory Hall alisema ,baada ya wiki mbili 
wataanza na zoezi la kuunganishia wale waliolipia Mbulani na kudai 
baadhi ya maeneo yapo kwenye mpango wa REA na kuwahakikishia umeme 
kwenye utafika katika maeneo aliyoomba mbunge Ulega ikiwemo shule za 
sekondari ,msingi na zahanati .
Mwenyekiti
 wa CCM Mkuranga,Ally Msikamo aliwataka wataalamu watoke maofisini na 
kwenda maeneo ya Vijijini kujionea uhalisia wa changamoto zinagusa 
wananchi.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...