Na
Mapuli Misalaba, Shinyanga
Wakazi
wa Kata ya Kitangili katika Manispaa ya Shinyanga wamewaomba viongozi wa ngazi
zote kuchukua hatua za haraka za kukabiliana na matukio ya Fisi kushambulia
watoto na kisha kuwasababishia vifo.
Wameyasema
hayo leo wakati wa maombolezo ya kifo cha mtoto Albert Shija mwenye umri wa
miaka 2 na miezi 10 aliyeuawa kwa kushambuliwa na Fisi juzi Jumamosi majira ya
saa moja usiku katika mtaa wa Imalilo kata ya Kitangili.
Wananchi
hao wamesema matukio ya watoto kuuawa na Fisi yameongezeka hali inayosababisha
hofu na taharuki kubwa kwa wakazi hao ambao wameomba mamlaka husika zichukue
hatua za haraka ili kukabiliana na hali hiyo inayotishia usalama
Diwani
wa kata ya Kitangili Mhe. Mariam Nyangaka amekiri kuwepo kwa taharuki inayosababishwa
na matukio hayo ambapo ameeleza kuwa ameitisha kikao maalumu kitakachohusisha
makundi mbalimbali ya wadau watakaojadili jinsi ya kutatua changamoto hiyo.
“Hatua
za moja kwa mojani kwamba kesho tunakutana na wazee maarufu, viongozi wa dini,
wazee wa mila tutawashirikisha kila nzengo tutakutana nao tujaribu kuangalia
namna ya kutatua suala hili tunafanyaje ili wananchi wakae kwa amani”
Diwani
huyo ametoa wito kwa wananchi wa Kata ya Kitangili kuchukua tahadhari ya
kuwalinda watoto dhidi ya mazingira hatarishi ili kuwaepusha na matukio ya aina
hiyo.
“wazazi tuwemakini kuwalinda watoto watoto wetu hasa muda wa jioni kuanzia Saa kumi na mbili mzazi uhakikishe mtoto yupo nyumban lakini pia wazazi wawe na namba za simu za viongozi kingine wananchi wawe na vitendea kazi mfano vipenga au panga vitu ambavyo wataweza kujihami"
Kwa
upande wa Idara ya maliasili, misitu na nyuki ya Halimashauri ya Manispaa ya
Shinyanga kwa kushirikiana na mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania TAWA
kanda ya Mwanza wameanza opareisheni malumu ya kuwasaka wanyamapori aina ya
Fisi ili kuthibiti matukio ya vifo na majeruhi.
Akizungumza
Afisa misitu wa Halmashauri ya Manispaa James Mduma amesema kuwa operation hiyo
imeanza kufuatia mfululizo wa matukio ya Fisi kujeruhi na kuua katika
maeneombalimbali ya Manispaa ya Shinyanga ikiwemo kata ya Kitangili.
Mduma
amefafanua zaidi kuwa utekelezaji wa oparesheni hiyo unafanyika kwa
kushirikiana na maafisa wa mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania TAWA
kanda ya Mwanza.
"Naamili
tunaweza tukafanya vizuri tukishirikiana na taasisi ya wanyamapori TAWA
tumekwisha kuwa na mawasiliano nao lakini kwa matukio haya mawili wamekuja na
hata sasa tukonao wanaendelea na operation kwa maana ya kwamba tuwasake hao
fisi wanaofanya hayo matukio kwahiyo tukishirikiana na ofisi ya wanyamapori
litadhibitiwa na ndiyo maana tunafanya kazi kwa kurikiana nao vizuri"
Akizungumzia
suala hilo Afisa Mhifadhi wanyamapori Daraja la Pili kutoka kikosi dhidi ya
ujangili, Mwanza Mohamed Mpoto ambaye ni mmoja kati ya Askari wanaoendesha
msako dhidi ya Fisi amefafanua kuhusu sheria ya wanyamapori inayohusisha
madhara yatokanayo na mazingira hatarishi ya wanyama wakali
"Mamlaka
ya wasimamizi wa wanyamapori Tanzania kupitia
mkurugenzi wa idara ya wanyamapori
sheria namba tano (5) ya mwaka 2009 ya wanyamapori imeainisha
wanyamapori wakali na waharifu na moja wapo ni fisi kwa kulitambua hilo sheria
imeainisha madhara ambayo atasababishiwa mwananchi aidha kuuawa au kujeruhiwa
Kuna kifuta machozi kwa kifo inatolewa shilingi Milioni moja, majeruhi shilingi
laki tano, Ng'ombe mmoja ni shilingi elfu hamsini lakini Mbuzi ni shilingi elfu
ishilini na tano (25,000)"
Opareisheni
hiyo inayoendelea katika Manispaa ya Shinyanga inafuatia kukithiri kwa
matukio ya kuuawa na kujeruhiwa kwa
wananchi hasa watoto wadogo katika maeneo mbalimbali katika kipindi cha mwaka
huu 2021.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...