Jeshi la Polisi mkoa wa Njombe linawashikilia Raia Hamsini na moja wanaotajwa kuwa ni wahamiaji haramu kutoka nchi mbalimbali Ikiwemo Ethiopia na Malawi.
Raia hao wamekamatwa katika kijiji cha Igando halmashauri ya wilaya ya Wanging'ombe Kilomita chache kabla ya kuingia Mpakani mwa mikoa ya Njombe na Mbeya.
Kamishna msaidizi wa Polisi Hamis Issa amekiri kuwashikilia raia hao na kueleza kwamba wamefanikiwa kuwakamata baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wananchi wazalendo
Issa ameongeza kuwa Raia hao walitelekezwa na Lori ambalo halijatambulika kwa haraka baada ya kutokomea nyakati za usiku baada ya kuwashusha raia hao walioeleza kutolewa Mkoani Tanga.
Jeshi la polisi mkoa wa njombe linaendelea na jitihada za kuutambua mtandao wa usafirishaji bin adam ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani Raia hao zaidi ya Hamsini waliokamatwa kwaajili ya Hatua zaidi za Kisheria
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...