Afisa Utumishi Mkuu kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Bw. Stanley Madyaga, akiwaasa watumishi wapya wa Sekta hiyo (hawapo pichani), kufanya kazi kwa ubunifu na nidhamu wakati wa semina elekezi iliyofanyika jijini Dodoma.
Afisa Utumishi kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Bi. Hindu Augossy (kulia), akizungumzia umuhimu wa watumishi wapya kufuata maadili ya utumishi wa umma katika semina elekezi iliyoandaliwa na Sekta hiyo kwa waajiriwa wapya jijini Dodoma. Kushoto ni Bi. Esther Mwina, Afisa Utumishi akifuatilia.
Baadhi ya watumishi wapya wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), wakifuatilia semia elekezi kutoka kwa mtaalam kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma (hayupo pichani), jijini Dodoma.
Afisa Utumishi Mkuu kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Bw. Stanley Madyaga (wan ne kushoto), katika picha ya pamoja na watumishi wapya wa Sekta hiyo mara baada ya kufungua rasmi semina elekezi, jijini Dodoma.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...