Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda akifurahia jambo pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Bi Kate Somvongsiri mara baada ya kumaliza mazungumzo katika Ofisi za Wizara ya Kilimo zilizopo Jijini Dodoma, tarehe 28 Octoba 2021. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Bi Kate Somvongsiri akimkabidhi zawadi mwenyeji wake
Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Bi Kate Somvongsiri mara baada ya kujadili kwa kina juu ya ushirikiano wa sekta ya kilimo katika kikao kazi kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Kilimo zilizopo Jijini Dodoma, tarehe 28 Octoba 2021.
Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda akimueleza Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Bi Kate Somvongsiri kuhusu

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma

Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda tarehe 28 Octoba 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Bi Kate Somvongsiri katika Ofisi za Wizara ya Kilimo zilizopo Jijini Dodoma.

Katika mazungumzo hayo wamejadili kwa kina kuhusu vipaombele vya serikali katika wizara ya kilimo.

Pia wamejadili umuhimu wa kutatua tija na uzalishaji mdogo kwenye mazao ya wakulima ili kutafuta muarobaini wa kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya kilimo nchini.

Kadhalika wamejadili umuhimu wa kuongeza nguvu na umuhimu katika sekta ya utafiti ili kubaini nini kinahitajika katika ardhi ya kilimo katika maeneo mbalimbali ya wakulima nchini ili wakulima waweze kutambua mazao yanayokubalika katika maeneo yao pamoja na kutambua aina na kiasi cha mbolea kinachohitajika.

Vilevile majadiliano hayo yamejikita Zaidi kuhusu umuhimu wa kuboresha huduma za ugani, ambapo Waziri Mkenda ameeleza kuwa tayari wizara yake imeanza kuchukua hatua madhubuti ikiwa ni pamoja na kuwawezesha maafisa ugani kuwa na Pikipiki ambazo zitawarahisishia kuwafikia wakulima kwa wakati.

Aidha, katika mazungumzo hayo wamejadili umuhimu wa Ugharamiaji wa kilimo (Agro Financing), pamoja na kuwekeza kwenye Kilimo Anga.

Mkurugenzi Mkazi wa USAID Bi Kate Somvongsiri amemueleza mwenyeji wake Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda kuwa USAID dhamira ya kushiriki katika kikao kazi hicho ni pamoja na kukutana nae ili kujitambulisha kwake kujua vipaombele vya Wizara na kuandaa mkakati wa namna ya kushirikiana na serikali katika kutatua changamoto za Kilimo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...